• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika


Utangulizi

Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika katika robo ya pili imetekeleza shughuli zifuatazo; Usambazaji wa pembejeo zenye ruzuku ya serikali, Kutoa ushauri wa kitalaamu juu ya kanuni bora za kilimo, kuratibu na kusimamia miradi inayo husiana na kilimo, kuandaa taarifa mbalimbali za kilimo na kuziwasilisha katika ngazi zinazohusika na kushirikiana na idara nyingine (maendeleo ya jamii, maliasili ardhi na misitu) Pamoja taasisi/mashirika ya RERAI na BTC katika kutekeleza masuala mtambuka.

USAMBAZAJI WA PEMBEJEO

Usambazaji wa pembejeo zenye ruzuku ya Serikali zilifika tarehe 3/12/2016 na kuanza kusambazwa vijijini tarehe 12/12/2016 baada ya mgao kwa vijiji 44 ndani ya Wilaya ya Kakonko uliofanywa na Kamati ya Pembejeo ya Wilaya. Katika mgao huo kila kijiji kilipata mgao wa mifuko arobaini (40) isipokuwa kijiji cha Nyakayenzi na Kinonko ambavyo vilipata mifuko sitini (60) kila kimoja. Gharama ya kuchangia toka kwa mkulima ni Shs.29,500/= kwa mfuko wa kilogram 50.

Hadi Kufikia tarehe 04/01/2017 jumla ya tani 77.45 (mifuko 1549), kati ya tani 90 (mifuko 1,800) za mbolea ya kukuzia (UREA) imefikishwa katika vijiji 42 kati ya vijiji 44. Vijiji vya Njomulole na Kihomoka bado.

Kihomoka; Mwenyekiti wa kamati ya pembejeo Wilaya ya Kakonko alikiondoa kijiji hiki katika kupata pembejeo kutokana na walengwa kukosa fedha za kuchangia (Shs.29,500/=) na kuamuru pembejeo hizo kupelekwa vijiji vya Kanyonza na Muganza vilivyopo ndani ya kata ya Kanyonza. Zoezi la Usambazaji bado linaendelea.

MAZAO;

  • Mazao ya Chakula

Shughuli kubwa inayoendelea vijijini kwa mazao ya chakula (Mahindi, Maharage, Muhogo, Mpunga, Mtama, Karanga, Viazi vitamu, mboga na matunda) ni upandaji, palizi na kuweka mbolea ya kukuzia.

Hali ya mzao kwa kipindi hiki inatofautiana katika vijiji, kutokana na maeneo mengi kuwa na uhaba wa mvua, hivyo mazao mengi kuanza kunyauka ingawa katikati mwa mwezi Desemba mvua ilinyesha na kuleta matumaini kwa baadhi ya mazao.

Kutokana na hali hiyo, Halmashauri ilitoa tahadhari kwa wananchi juu ya uwezekano wa kuwepo kwa upungufu wa Chakula msimu huu na kuwashauri kutumia chakula kilichopo kwa uangalifu mkubwa na pia kupanda mazao yanayokomaa mapema na kuvumilia ukame kama vile Viazi vitamu, Mtama na Mihogo ili kukabiliana na upungufu huo wa chakula unaoweza kujitokeza.

  • Mazao ya Biashara
  • Pamba
  • Kwa zao la pamba, shughuli iliyofanyika ni uuzaji wa mbegu za pamba kwa wakulima na upandaji, hamasa kwa wakulima juu ya kilimo cha Pamba kwa kutumia mikutano na ushauri wa wataalam wa kilimo na Viongozi.
  • Changamoto zilizojitokeza ni pamoja kukoseka kwa mvua wakati wa majira ya kupanda, mkanganyiko juu ya utaratibu wa uuzaji wa mbegu za pamba aidha kwa wakulima kukopeshwa au kununua taslimu.
  • Kwa Maelekezo ya bodi ya pamba ilikuwa ni kuuza mbegu hiyo kwa njia ya kukopesha au tasilimu, lakini muuzaji wa mbegu ambaye ni Kampuni ya KCCL (Kahama Cotton Company Ltd) baadaye hakuwa tayari kuuza mbegu kwa kuwakopesha wakulima na kuwataka wanunue tasilimu, hali iliyopelekea wakulima wengi kushindwa kununua mbegu msimu huu. Hata hivyo tuliiandikia Bodi ya Pamba Kutoa ufafanuzi juu ya hilo, Majibu tuliyopewa na bodi ni kwamba utaratibu ni kuwa wakulima watauziwa kwa njia ya kukopeshwa au fedha taslimu.
  •  Tumbaku:
  • Zao hili kwa ujumla husimamiwa na bodi ya Tumbaku kwa kutumia makampuni mbalimbali yasiyo ya kiserikali, hivyo  idara kupitia kitengo cha Ushirika na maafisa ugani hushirikiana na Makampuni hayo kutoa elimu kwa wakulima wa tumbaku kama ilivyo kwa mazao mengine.
  • Kahawa:
  • Shughuli inayoendelea kwa zao hili ni Palizi ya mashamba, pia kupanda/kuotesha miche mipya ya kahawa ambapo hadi sasa ushirika wa kahawa Muhange (MUCPA) wamepandikiza vikonyo/miche 600.
  • Hali ya zao hili kwa sasa ni nzuri na hatua iliyofikia ni ya uzaaji na ikiwa hali ya hewa itaendelea vizuri tunatarajia kupata mavuno wastani wa kilo 40,600 (tani 40.6) za Kahawa. Usimamizi wa zao hili unaendelea kusimamiwa na chama cha msingi cha MUCPA.
  • Pia Halmashauri ilifanywa mkutano na wakulima hao na kuunda Uongozi wa mpito baada ya Uongozi uliokuwepo kushindwa kufanya kazi vizuri na kusababisha kuzorota kwa shughuli za ushirika huu.
  • Uzalishaji wa mbegu za Muhogo:
  • Kwa zao la muhogo, Halmashauri inaendelea na uzalishaji wa mbegu za muhogo chini ya mradi wa SAKIP (Sustainable Agiculture Kigoma Region Project) chini ya shirika la BTC na  jumla ya tani kumi (10) za mbegu ya muhogo aina ya Mkombozi na ilisambazwa kwa vikundi vitano (5) vya wakulima na mkulima mmoja mmoja wakulima sita(6) na kupandwa katika jumla ya eneo la wastani wa ekari ishirini na tano (25) kama inavyo onesha hapa:-                                                       (Jedwali Na.2 hapa chini linaonyesha).
  • Uzalishaji wa mbegu hizi utasaidia kukabiliana na tatizo la ugonjwa wa Bato bato kali na Michirizi Kahawia kwa kuwa mbegu hiyo haishambuliwi na magonjwa hayo.
  • MKULIMA MMOJA MMOJA
S/N
MKULIMA MMOJA MMOJA/VIKUNDI
IDADI YA WAKULIMA
ME
KE
IDADI YA MIFUKO YENYE UJAZO WA PINGILI 1000
KIJIJI

ENEO/EKARI

NAMBA YA SIMU

1

JUMA MAGANGA

1

1


4

ITUMBIKO

1

0755-906050

2

SIMON KIPARA

1

1


4

ITUMBIKO

1

0764-217756

3

BENARD MICHAEL

1

1


4

ITUMBIKO

1

0765-820592

4

DEBORA TITUS

1

0

1

4

ITUMBIKO

1

0753-836162

5

JAPHET.BASEKILOLA

1

1


4

RUYENZI

1


6

SAMWELI NTAMBALA

1

1


4

RUYENZI

1



JUMLA

6

5

1

24

 

6

 
  •  
  •  
  • VIKUNDI VYA WAKULIMA

 
INA LA KIKUNDI
 
IDADI YA WAKULMA
 
ME
 
KE
IDADI YA MIFUKO  UJAZO PINGILI 1000
 
KIJIJI
 
ENEO/EKARI
 
NAMBA YA SIMU

1

TUMAINI

22

13

9

32

KIYOBERA

4

0765-836998
2
KINAMAMA TUSHIKAMANE

12

0

12

32

KIYOBERA

4

0755-090268
3
TUJITEGEMEE

14

0

14

32

MUGANZA

4

0769-646459

4

MWENDO WA SAA

25

12

13

23

KIGA

3

0624-389646

5

TUJIKWAMUE

25

0

25

24

KASONGATI

4

0621-383164

Jumla

98

25

73

143

 

19

 

 

USAMBAZAJI WA MBEGU ZA MAHARAGE 

Halmashauri kupitia idara ya Kilimo, robo hii imesambaza mbegu za Maharage kwa kushirikiana na Kampuni ya   QFP (Quality Food Product) ya Arusha. Mbegu hizo ziliuzwa kwa utaratibu wa mkopo kwa kutanguliza nusu ya malipo ya fedha TSh.1000/=, ambapo bei halisi ya kilo moja ilikuwa TSh. 2000/= kwa kilo moja. Jumla ya kilo 21,200 sawa na tani 21.2 za mbegu ya maharage yaliyouzwa kwa wakulima 600 na kupandwa katika Ekari 848.

USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MRADI WA MIVARF. 

MIVARF (Markenting Infrastructure,Value addition and Rural Fainance Supporting Programme) ni Mradi unao shughulika na Mnyororo wa thamani wa zao la Mpunga katika Wilaya ya Kakonko. Mradi huu unasaidia kutoa mafunzo kwa wakulima juu ya Kuongeza thamani ya mazao (Value addition), Kuwaunganisha wakulima na Masoko (Market Linkage) na Huduma za Kifedha vijijini (Rural Finance). Utekelezaji wa mafunzo hayo hufanyika lengu kuu la Kuwajengea uwezo wakulima katika uzalishaji na kuwaunganisha na masoko. (Producer Empowerment and Market Linkage- PEML)

 Kazi zilizotekelezwa katika idara ya Kilimo ni Usimamizi wa kazi zinazotekelezwa na mtoa huduma (SP) wa MIVARF ambaye ni Shirika la RERAI. Kazi hii ilifanyika kwa kushirikiana na Kamati ya Usimamizi wa Mradi ya Wilaya;- Shughuli zilizofanyika ni pamoja:-

  • Kutembelea vikundi vinavyotekeleza mradi wa MIVARF katika vijiji vya Nyamtukuza, Rumashi, Nyakayenzi na Kinonko na kufanya tathmini ya mafunzo yaliyotolewa.
  • Kufanya vikao vya kawaida vya tathmini ya kazi za mtoa huduma
  • Kuratibu kazi za mradi ngazi ya wilaya.
  • Kuandaa taarifa za mradi na kuziwasilisha kwa ngazi ya Mkoa na MIVARF- Taifa.

Taarifa ilijadiliwa na kupokelewa.

Matangazo

  • FORM I 2021 JOIN INSTRUCTIONS December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa stendi ya kisasa Kakonko waanza kutekelezwa kwa gharama ya Tsh.2.1 bilioni kwa siku 365

    June 20, 2019
  • Hospitali ya Wilaya ya Kakonko yapokea msaada wa vifaa tiba na madawa ya Tsh.88,295,430/=

    May 02, 2019
  • BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA AKABIDHI VIFAA VYA MIFUGO KAKONKO

    January 24, 2019
  • MIRADI 3 YA MAJI YA BILIONI 1.5 KUTEKELEZWA NDANI YA MIEZI 6 KAKONKO

    June 08, 2018
  • Tazama zote

Video

Maadhimisho ya siku ya wanawake kitaifa yafanyika kwa ufanisi Mkoani Simiyu Machi 8, 2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Pakua hati yako ya malipo ya mshahara Hapa "Utumishi Portal"
  • Tangazo la zabuni
  • Matokeo ya Mitihani ya baraza
  • Nafasi za kazi zinazotolewa na Sekretalieti ya Ajira
  • Taarifa kwa Umma zinazotolewa na "TAMISEMI"

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: 028-2820137

    Simu ya Mkononi: 0757470800

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa