• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Historia


WASIFU WA HALMASHAURI

1.0 Utangulizi

Wilaya ya Kakonko ilianzishwa kwa tangazo la Serikali GN. 287 ya mwaka 2011 baada ya kugawa Wilaya ya Kibondo na kuunda Wilaya ya Kibondo na Kakonko. Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ilianzishwa tarehe 08/3/2013 na kutangazwa katika gazeti la Serikali kwa GN.42.

Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya yapo katika mji wa Kakonko uliopo umbali wa Km 48 Kaskazini mwa mji wa Kibondo katika barabara kuu ya Kigoma – Mwanza.

1.1 Jiografia ya Mahali ilipo Wilaya

Kakonko ni Halmashauri moja wapo kati ya Halmashauri 8 za Mkoa wa Kigoma. Wilaya ipo upande wa kaskazini mwa mkoa wa Kigoma na inapakana na Wilaya ya Ngara na Biharamulo (Mkoa wa Kagera) kwa upande wa Kaskazini na Magharibi inapakana na Jamhuri ya Burundi, Kusini inapakana na Wilaya ya Kibondo, Mashariki hadi Kaskazini Mashariki inapakana na Wilaya ya Bukombe (Mkoa wa Geita).

1.2 Ukubwa wa Wilaya

Wilaya ya Kakonko ina ukubwa wa kilometa za mraba 7,715.05 ambazo zimegawanyika katika makundi sita ya matumizi kama inavyo onesha kwenye jedwali 1.1 hapa chini.

JEDWALI 1.1 UKUBWA WA ENEO LA WILAYA

FUNGU
MATUMIZI

KM2

ASILIMIA (%)
1
Mamlaka ya vijiji

2,041.03

26.5

2
Msitu wa hifadhi

178.65

2.3

3
Ardhi inayofaa kwa kilimo (ardhi inayolimwa ni KM2 671.8 sawa na 62%)

1,084.2

14.1

4
Malisho ya mifugo

806.4

10.5

5
Hifadhi ya akiba ya wanyamapori na misitu (Moyowosi Game Reserve and Buyungu Local Authority Forest Reserve)

624.9

8.1

6
Makazi, Huduma za Jamii, Milima na Maji

2,979.87

38.5

JUMLA

7,715.05

100

Chanzo: Idara ya Ardhi 

1.3 Idadi ya Watu 

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 Wilaya ya Kakonko ilikuwa na Jumla ya Watu 178,419   ambapo idadi ya wanaume ilikuwa 86,688 sawa na asilimia 49 na idadi ya wanawake ilikuwa 91,731 sawa na asilimia 51. Kasi ya ongezeko la watu katika   Wilaya ya Kakonko (Inter-censal Population Growth Rate) ni 0.6 kati ya Sensa ya watu mwaka 2012 ambapo idadi ya watu ilikuwa 167,555 na Sensa ya watu na makazi ya Mwaka 2022 ambapo idadi ya watu ni 178,419. Aidha Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya 2022 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ilikuwa na idadi ya Kaya 37,361 ambapo kulikuwa na wastani wa watu 4 kwa kaya. Mchanganuo wa Idadi ya watu, Kaya, Wastani wa watu kwa Kaya na wastani wa kijinsi ni kama ilivyo kwenye Jedwali 1.2 hapa chini

JEDWALI 1.2 IDADI YA WATU, KAYA, WASTANI WA IDADI YA WATU KWA KAYA NA WASTANI WA JINSI

HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO

Na
KATA

IDADI YA WATU

IDADI YA KAYA
WASTANI WA IDADI YA WATU KWA KAYA
WASTANI WA KIJINSI
JUMLA
ME
%ME
KE
%KE
 

  178,419 

 86,688 

49%

 91,731 

51%

   37,361 

4.8

95

1.
Nyabibuye

    10,162

    4,950

3%

    5,212

3%

     2,090

4.9

95

2.
Nyamtukuza

    20,612

 10,362

6%

 10,250

6%

     4,030

5.1

101

3.
Muhange

    10,246

    5,087

3%

    5,159

3%

     2,048

5.0

99

4.
Gwarama

    17,668

    8,645

5%

    9,023

5%

     3,775

4.7

96

5.
Kakonko

    14,629

    7,080

4%

    7,549

4%

     3,245

4.5

94

6.
Kiziguzigu

    13,025

    6,312

4%

    6,713

4%

     2,695

4.8

94

7.
Kanyonza

    10,608

    5,378

3%

    5,230

3%

     2,143

5.0

103

8.
Kasuga

    16,769

    8,198

5%

    8,571

5%

     3,401

4.9

96

9.
Rugenge

    11,257

    5,330

3%

    5,927

3%

     2,297

4.9

90

10.
Kasanda

    17,927

    8,611

5%

    9,316

5%

     3,691

4.9

92

11.
Gwanumpu

    14,956

    7,043

4%

    7,913

4%

     3,214

4.7

89

12.
Katanga

      9,701

    4,620

3%

    5,081

3%

     2,203

4.4

91

13.
Mugunzu

    10,859

    5,072

3%

    5,787

3%

     2,529

4.3

88

Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

 

 

1.4 Mgawanyo wa idadi ya watu kwa Umri, Jinsi na maeneo wanayoishi

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Mkazi ya mwaka 2022, takwimu zinaonyesha idadi kubwa ya watu ilikuwa wa umri kati ya miaka 0-4 ambapo idadi yao ilikuwa 31,121 sawa na asilimia 17% ya idadi ya watu wote. Vile vile idadi kubwa ya watu 173,113 sawa na asilimia 97 ni ambao wanaishi vijijini na watu 5,306 sawa na asilimia 3 wanaishi Mjini. Mchanganuo wa takwimu hizi upo katika jedwali 1.3 hapa chini

JEDWALI 1.3: MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI, JINSI NA MAENEO WANAYOISHI

Mgawanyo wa Idadi ya Watu kwa Umri, Jinsi na Maeneo wanapoishi

UMRI

JUMLA

WANAOISHI VIJIJINI

WANAOISHI MJINI

JUMLA

% mgawanyo wa idadi nya watu kwa umri

Me

Ke

Me

Ke

Jumla

% ya wanaoishi vijijini

Me

Ke

Jumla

% ya wanaoishi Mjini

JUMLA

178,419


86,688

91,731

84,135

88,978

173,113

97

2,553

2,753

5,306

3

0 - 4

31,121

17

15,671

15,450

15,325

15,087

30,412


346

363

709


05.-09

28,697

16

14,171

14,526

13,863

14,202

28,065

308

324

632

10.-14

27,207

15

13,760

13,447

13,420

13,084

26,504

340

363

703

15 - 19

18,262

10

9,283

8,979

8,986

8,627

17,613

297

352

649

20 - 24

13,612

8

6,186

7,426

5,927

7,160

13,087

259

266

525

25 - 29

11,063

6

5,175

5,888

4,972

5,610

10,582

203

278

481

30 - 34

8,875

5

4,289

4,586

4,070

4,383

8,453

219

203

422

35 - 39

7,696

4

3,598

4,098

3,443

3,967

7,410

155

131

286

40 - 44

6,459

4

3,000

3,459

2,898

3,361

6,259

102

98

200

45 - 49

5,877

3

2,723

3,154

2,629

3,052

5,681

94

102

196

50 - 54

5,014

3

2,327

2,687

2,253

2,619

4,872

74

68

142

55 - 59

3,673

2

1,750

1,923

1,696

1,860

3,556

54

63

117

60 - 64

3,567

2

1,702

1,865

1,658

1,817

3,475

44

48

92

65 - 69

2,175

1

993

1,182

966

1,152

2,118

27

30

57

70 - 74

1,928

1

831

1,097

815

1,069

1,884

16

28

44

75 - 79

1,148

1

485

663

475

650

1,125

10

13

23

80+

2,045

1

744

1,301

739

1,278

2,017

5

23

28

Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

1.5: Hali ya Hewa

Hali ya hewa ni nyuzi joto kati ya 150C hadi 220C na hupata mvua kati ya 800mm hadi

1,900mm kwa mwaka kuanzia mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi mwisho wa Mei.

2.0 Sekta ya Utawala

Wilaya ya Kakonko ina jumla ya Tarafa tatu (3) ambazo ni Nyaronga, Kasanda na

Kakonko ambazo zina jumla ya Kata kumi na tatu (13), vijiji 44 na Vitongoji 355.

Utawala bora na uwajibikaji ni mojawapo ya maeneo muhimu yanayopewa kipaumbele na Serikali kupitia Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, Dira ya maendeleo ya Taifa 2025, Mkakati wa Maendeleo Endelevu (SDG) na Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano (2021/2022 – 2025/2026).

Kero na malalamiko mbalimbali ya wananchi hutatuliwa kupitia Ofisi za Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji, Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wa Kata, Mkurugenzi Mtendaji, Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Aidha Halmashauri ina dawati maalumu linaloshughulikia malalamiko mbalimbali yanayoletwa dhidi ya Halmashauri au Watendaji wake na kufanya ufuatiliaji kuhakikisha kila lalamiko la mwananchi linatatuliwa au kuelekezwa kwenye mamlaka inayohusika. Baadhi ya malalamiko ama kero ni kama Migogoro ya Ardhi, Migogoro ya unyanyasaji wa Kijinsia na mingine. Kero nyingi hutatuliwa kupitia dawati la malalamiko kwa kuwasiliana ama kushirikiana na wahusika wa maeneo au idara husika. Pia masanduku ya maoni yamewekwa katika ofisi ili kubaini kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi mapema.

2.1 Hali ya Watumishi katika Halmashauri

Kwa mwaka 2022/2023, Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ina jumla ya Watumishi 1199 kati ya mahitaji ya watumishi 1958 ambapo upungufu wa watumishi ni 759 sawa na asilimia 39. Aidha katika watumishi waliopo idadi ya watumishi wa jinsia ya kiume ni 834 sawa na asilimia 70 na watumishi 365 ni wa jinsia ya Kike sawa na asilimia 30. Hali ya watumishi kwa miaka mitatu ni kama inavyoonekana kwenye jedwali 1.4 hapa chini.

JEDWALI 1.4: HALI YA WATUMISHI 

HALI YA WATUMISHI
MGAWANYO WA WATUMISHI WALIOPO KIJINSI (2022/2023)
MWAKA
MAHITAJI
WALIOPO
UPUNGUFU
% UPUNGUFU
ME
%ME
KE
%KE
2020/2021

1958

951

1007

51





2021/2022

1958

988

970

50





2022/2023

1958

1199

759

39

834

70

365

30

Chanzo: Idara ya Utawala na Utumishi

2.2 Watumishi wapya walioajiriwa katika kipindi cha miaka mitatu.

Katika Kipindi cha miaka mitatu 2020/2021, 2021/2022 na 2022/2023 Halmashauri imefanikiwa kupata ajira mpya 303 kwa Kada tofauti tofauti ambapo watumishi wengi walioajiriwa ni wa Idara ya elimu msingi ambao walikuwa 122 sawa na asilimia 40.26, idara ya afya watumishi 80 sawa na asilimia 26.40, Idara ya Elimu Sekondari watumishi 60 sawa na asilimia 19.80, idara ya Utawala watumishi 40 sawa na asilimia 13.20 na idara ya Ujenzi Mtumishi 1 sawa na asilimia 0.33. Mchanganuo wa watumishi walioajiriwa ni kama ilivyo kwenye jedwali 1.5 hapa chini

JEDWALI 1.5: WATUMISHI WAPYA WALIOAJIRIWA 2020/2021-2022/2023

WATUMISHI WAPYA WALIOAJIRIWA
MWAKA
IDADI YA WATUMISHI WALIOAJIRIWA
IDARA YA UTAWALA
IDARA YA AFYA
IDARA YA ELIMU MSINGI
IDARA YA ELIMU SEKONDARI
IDARA YA UJENZI
2020/2021

34

1

0

17

16

0

2021/2022

107

0

44

36

26

1

2022/2023

162

39

36

69

18

0

JUMLA

303

40

80

122

60

1

%WATUMISHI KWA IDARA

 

13.20

26.40

40.26

19.80

0.33

Chanzo: Idara ya Utawala na Utumishi

Halmashauri imekuwa ikitenga bajeti kwa ajili ya ajira mpya kwa kila mwaka wa fedha ili kuhakikisha Halmashauri inaweza kupata watumishi wa kutosha ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi.

2.3 Ujenzi wa nyumba za Watumishi

Katika kipindi cha miaka mitatu Halmashauri imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa idara 1 na inaendelea na ujenzi wa nyumba 1 ya Wakuu wa Idara ambapo mpaka kufikia mwezi Juni 2023 ujenzi wa nyumba mbili za wakuu wa idara umefikia hatua ya umaliziaji kwa nyumba moja na hatua ya msingi kwa nyumba ya pili.

2.4 Ujenzi wa Majengo ya Utawala

Katika kipindi cha 2019/2020 hadi 2022/2023 Halmashauri imendelea na ujenzi wa jengo la utawala ambapo mpaka kufikia Juni 2023 ujenzi wa ukumbi upo katika hatua ya kunyanyua boma. Kukamilika kwa mradi huu kutaongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa wananchi.

2.5 Mkakati wa kuwabakiza watumishi

Halmashauri ameandaa mkakati wa kuwabakiza watumishi ili kupunguza idadi ya watumishi wanaohama kwa kufanya yafuatayo:

2.5.1 Kutoa motisha kwa watumishi wapya.

  • Kuwepo kwa malazi, chakula na viburudisho wakati wa mapokezi.
  • Kuwepo kwa mapokezi na usafiri kutoka stendi kuu ya wilaya ya Kakonko.
  • Uwepo wa nyaraka mbalimbali zinazohusiana na ajira.
  • Matumizi ya lugha nzuri kwa watumishi wapya wakati wa mapokezi.
  •  Fedha za kujikimu kwa watumishi wapya kutolewa kwa wakati.
  • Masuala yahusuyo mishahara kushughulikiwa kwa wakati
  • Kutengeneza mazingira rafiki ya upatikanaji wa viwanja vya makazi kwa kuwapunguzia kuanzia asilimia 20-30; iliwahamasike kujenga nyumba zao na hatimaye wayafanye makazi yao ya Kakonko kuwa ya kudumu.
  • Kuwepo kwa usafiri wa kuwapeleka watumishi wapya kwenye vituo vyao vya kazi.
  • Mwajiri kutoa Lori kwa watumishi wanaojenga ili wao wagharimie mafuta wakati wa kusomba vifaa vyao vya ujenzi.

2.5.2 Watumishi waliopo.

  • Kutolewa kwa mikopo nafuu.
  • Kutengeneza mazingira rafiki kati ya watumishi na jamii inayowazunguka kwa kuwepo kwa kikosi kazi maalum kitakachozunguka wilaya nzima.
  • Kuboresha utoaji wa huduma/utoaji wa huduma kwa wakati.
  • Kuwepo kwa mabonanza mbalimbali ya michezo ili kuondoa ombwe lililopo kati ya watumishi wa makao makuu na wale waliopo kwenye vituo vya kutolea huduma.
  • Kutengeneza mazingira rafiki ya upatikanaji wa viwanja vya makazi.
  • Kuwatambua watumishi wanaofanya vizuri katika kazi zao na kuwapa motisha mbalimbali kama vile kupelekwa sehemu za utalii na kupewa madaraka.
  • Uwepo wa usafiri wakuwapeleka kazini na kuwarudisha watumishi wa Makao Makuu.
  • Mwajiri kuwapunguzia watumishi bei za viwanja ili wahamasike kujenga nyumba zao na hatimaye wayafanye makazi yao ya Kakonko kuwa ya kudumu.
  • Mwajiri kutoa lori kwa watumishi wanaojenga ili wao wagharimie mafuta wakati wakusomba vifaa vyao vya ujenzi.
  • Mwajiri kujenga hosteli/Nyumba ya kulala wageni ya biashara kwaajili ya kuiingizia Halmashauri mapato ambapo pia itatumika kuwapokelea watumishi wapya
  • Halmashauri kutengeneza maeneo mbalimbali ya starehe yatakayowafanya watumishi na familia zao kuwa na sehemu za kupumuzika na kufurahi kama ilivyo miji mingine.
  • Kutoa mafunzo kwa watumishi wanaotarajiwa kustaafu kazi kwa kuwapatia mbinu mbalimbali za namna ya kuishi baada ya kustaafu.

3.0 Uandikishaji wa Anwani za Makazi.

Wilaya ya Kakonko imetekeleza kikamilifu zoezi la uandikishaji wa Anwani za Makazi ambapo jumla ya nyumba 43,386 sawa na 100% ya malengo ya uandikishaji zimefikiwa na zoezi la uhakiki wa taarifa limekamilika. Zoezi la uwekaji wa namba za nyumba zilizotambuliwa limekamilika kwa asilimia 100 na zoezi la uwekaji wa majina ya Mitaa umekamilika. Zoezi hili limesaidia sana na kurahisisha utambuzi wa makazi na kufikiwa kwa urahisi tofauti na hapo awali. Jumla ya Sh.100,895,505.99 zilipokelewa kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya kuendesha zoezi na zimetumika.



4.0 Mapato

4.1 Mapato ya Halmashauri

Vyanzo vikuu vya mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ni kutoka Serikali kuu, Fedha za wadau wa maendeleo, mapato ya ndani na wahisani mbalimbali. Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 makusanyo ya mapato ya ndani yameongezeka kutokana na kuongezeka kwa makusanyo ya ushuru wa soko pamoja na makusanyo kutoka mradi wa Matofali

Mwenendo wa makusanyo ya mapato ya ndani kupitia vyanzo mbalimbali pamoja na mapokezi ya fedha za ruzuku toka Serikali Kuu kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2020/2021 hadi 2022/2023 kwa wastani ni ya kuridhisha kama inavyoonesha kwenye Jedwali 1.6 hapa chini.

JEDWALI 1.6: MUHTASARI WA MAPATO KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021-2022/2023

Mwaka
Bajeti Kiasi TZS
Makusanyo
Asilimia
2020/2021

1,031,933,256.00

842,746,697.00

82

2021/2022

1,038,636,000.00

1,069,058,023.00

103

2022/2023

1,142,499,600.00

   1,192,450,028.45

104

Chanzo: Taarifa ya fedha

4.2 Udhibiti wa matumizi ya Fedha za Serikali

Halmashauri imeendelea kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika matumizi ya fedha za Serikali. Kutokana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha miaka mitatu (3) iliyopita Halmashauri imeweza kupata hati tofauti kama ilivyo kwenye jedwali 1.7 hapa chini:

JEDWALI 1.7: HALI YA HATI ZA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI

Mwaka
Aina ya Hati
2020/2021
Hati yenye mashaka
2021/2022
Hati safi
2022/2023
 Ukaguzi unaendelea

Chanzo: Ripoti ya Mdhibiti Na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko inayo mikakati mbalimbali ya kuendelea kupata hati safi, ikiwa ni pamoja na:

  • Ukamilishaji wa utekelezaji wa shughuli na miradi ya maendeleo unaokwenda sambamba na upokeaji wa fedha na matumizi sahihi
  • Uandaaji wa hesabu kwa kufuata taratibu na kanuni za fedha

5.0 Utekelezaji Sekta za Uzalishaji na Huduma za Kijamii

5.1.0 Sekta ya Kilimo

Wilaya ya Kakonko ina eneo linalofaa kwa kilimo jumla ya Hekta 108,420.14 sawa na 14.1% ya eneo la Wilaya, kwa msimu wa 2019/2020 eneo limwa lilikuwa hekta 67,220.49 sawa na 61.9% ya ardhi inayofaa kwa kilimo, ambapo kwa msimu wa kilimo 2021/2022 eneo limwa limeongezeka na kufikia jumla ya Hekta 98,459.5 za mazao ya chakula na biashara sawa na ongezeko la 46.47%. Mazao yanayostawi na kulimwa ni pamoja na Mahindi, Maharage, Karanga, Migomba, Mpunga, Tumbaku, Pamba, Mtama, Kahawa, Alizeti, Mhogo, Viazi vitamu na Mazao ya bustani. Aidha Wilaya ina jumla ya wastani wa kaya  31,010 za kilimo sawa na 83% ya kaya 37,361 zilizopo Wilayani. Kilimo ni shughuli kuu ya uchumi na kwa kiasi kikubwa kinategemea mvua na umwagiliaji kwa kiasi kidogo.

5.1.1 Usalama wa Chakula 

Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2022/2023 Wilaya ya Kakonko imevuna wastani wa mazao ya chakula kinachotosheleza mahitaji ya watu waliopo Wilayani na kubakiwa na ziada. Jedwali 1.8 linaonesha mchanganuo wa mahitaji, mavuno na ziada kwa kipindi tajwa.

JEDWALI 1.8 MCHANGANUO WA MAHITAJI, MAVUNO NA ZIADA YA CHAKULA KWA MWAKA 2020/2021-2022/2023

Mwaka
Mahitaji (Tani)
Mavuno (Tani)
Ziada (Tani)
2020/2021

70,965.08

191,875.35

120,910.27

2021/2022

76,374.51

157,746.82

81,372.31

2022/2023

71,791.24

270,546.86

198,755.62

  Chanzo: Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

 

  JEDWALI 1.9 MCHANGANUO WA USALAMA WA CHAKULA KWA MWAKA 2023


 IDADI YA WATU 178,419 


 mahitaji (Tani)
 mavuno (Tani)
 ziada (Tani)
 wanga

         66,907.13

      241,552.86

  174,645.73

 protini

           4,884.11

         28,994.00

     24,109.89

JUMLA YA ZIADA 

  198,755.62 

                                   

Chanzo: Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

 

Kwa mwaka 2023 hali ya mahitaji ya chakula imeshuka kwa sababu kwa miaka ya nyuma makadirio ya mahitaji ya chakula kufanyika kwa kutumia takwimu za makisio ya idadi ya watu ambapo makisio ya idadi ya watu yalikuwa watu 185,977 ila kwa mwaka 2023 makadirio ya mahitaji ya chakula yametumia idadi kamili ya watu ambayo kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi idadi ya watu Halmashauri ya Kakonko ni 178,419


 

5.1.2 Pembejeo za Kilimo

Hali ya upatikanaji wa pembejeo ni ya wastani kutokana na Kukosekana kwaWafanyabiashara wakubwa wa pembejeo ndani ya Wilaya.  Msimu wa mwaka 2021/2022 kulikuwa na wauzaji wadogowadogo 7 wa pembejeo za kilimo na kwa msimu wa 2022/2023 idadi imeongezeka na kufikia 9 ambapo kati ya 1 tu ndo aliruhusiwa kufanya biashara ya mbolea ya ruzuku.

5.1.3 Miradi ya Kilimo.

Halmashauri inashirikiana na wadau wa maendeleo ya kilimo kupitia mashirika ya Enabel kwa Mradi wa SAKiRP na Mashirika ya Umoja wa Mataifa (FAO, WFP, UNCDF na ITC) kupitia Mradi wa Pamoja Kigoma (KJP) kuendeleza kilimo Wilayani. Kupitia Mpango  huu,  kwa  msimu  wa  2020/2021  hadi  2022/2023  jumla  ya  kata  10  za Gwanumpu, Gwarama, Kanyonza, Kasanda, Kakonko, Mugunzu, Katanga, Rugenge, Muhange na Kasuga zimenufaika kwa kuwapatia mafunzo juu ya Mbinu bora za kilimo, zana za kilimo, Kilimo hifadhi na kilimo kinachoendana na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na ujenzi wa miundombinu ya kilimo ambayo ni Kituo cha mazao Kabingo, Ujenzi wa madaraja ya kusafirishia mazao Kata ya Kasanda, Gwarama na Kasuga na Ghala la mazau Kata ya Mugunzu

5.1.4 Umwagiliaji

Halmashauri ina jumla ya Skimu za Umwagiliaji 7 zenye eneo lililopimwa lenye ukubwa wa hekta 1,150. Aidha eneo linalolimwa ni hekta 935 na kuajiri wakulima 1,656. Pamoja na kuendelea na uzalishaji, miundombinu ya skimu hizi inatarajiwa kufanyiwa ukarabati kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ikiwa ni pamoja na ujenzi wa skimu nyingine mpya nne.

5.1.5 Ushirika.

Wilaya ina jumla ya vyama vya ushirika 15, ikiwa 14 ni vyama vya Msingi vya mazao na masoko (AMCOS) na 1 ni chama cha msingi cha akiba na mikopo (SACCOS). Vyama hivyo vina jumla ya wanachama 1,794.

5.2 Sekta ya Mifugo na Uvuvi

5.2.1 Mifugo

Ufugaji unaofanywa ni ufugaji huria na ufugaji wa ndani kwa kiasi kidogo. Wilaya ina jumla ya hekta 80,640.2 za eneo la malisho ambazo zinapatikana katika maeneo ya Vijiji 44 vya Wilaya ya Kakonko yaliyotengwa kwa ajili ya kuchungia. Kwa sasa Wilaya inakadiriwa kuwa na mifugo kama inavyoonesha kwenye jedwali 1.10 hapa chini: -

JEDWALI 1.10 : IDADI YA MIFUGO NDANI YA WILAYA.

Idadi na Aina ya mifugo
Mwaka
Ng’ombe
Mbuzi
Kondoo
Nguruwe
Bata
Kuku
Mbwa
Paka
Punda
2020/2021

24,863

28,219

694

2,134

1,230

68,316

1,527

81

31

2021/2022

26,518

30,311

859

2,742

1,596

79,672

2,059

89

35

2022/2023

27,635

32,918

933

2,925

1,640

81,416

2,063

85

41

Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi.

5.2.1.1 Ujenzi na ukarabati wa miundombinu

Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 hadi 2021/2022, Halmashauri kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanikiwa kujenga majosho 7 ya Nyamtukuza, Nyakayenzi, Kihomoka, Gwarama, Nyabibuye, Luhuru na Kasanda kwa gharama ya jumla ya Sh.126,000,000.00 ambapo kila josho moja limegharimu Sh.18,000,000.00 kujengwa. Majosho 7 yamejengwa na kukamilika.

Kwa mwaka 2022/23 majosho matano yako kwenye hatua za mwisho za ukamilishaji katika vijiji vya Kiduduye, Ilabiro, Kikulazo, Kiziguzigu na Itumbiko kwa gharama ya Tsh. 23,000,000/= kila moja na kufanya jumla ya gharama ya majosho yote matano kuwa Tsh. 115,000,000/=

5.2.1.2 Utengaji wa maeneo ya malisho

Halmashauri imetenga eneo la malisho ya mifugo katika vijiji saba (7) kati ya Vijiji 44 lenye ukubwa wa hekta 15,338 katika Vijiji vya Kazilamihunda, Juhudi, Kabare, Gwarama, Rumashi, Nyabibuye na Churazo kwa mipango wa matumizi bora ya Ardhi ya vijiji chini ya ufadhili wa shirika la Ubelgiji la Enabel.

5.2.1.3 Kuimarika kwa Huduma za Ugani kwa Wafugaji.

Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2022/2023 Halmashauri imefanikiwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za Ugani mfano utoaji chanjo (chambavu, Kideri Homa ya Mapafu ya Ng’ombe na Kichaa cha Mbwa) kwa wastani kutoka asilimia 50 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 80 mwaka 2023.

5.2.1.4 Hali ya Chanjo ya mifugo

Katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo, Halmashauri imekuwa ikifanyo zoezi la kutoa chanjo kwa kwa ajili ya kinga ya magonjwa mbalimbali ya mifugo kama inavyoonekana kwenye jedwali 1.11 hapa chini; -

JEDWALI 1.11: Chanjo ya mifugo Kwa kipindi cha Januari 2020 hadi Juni 2023

AINA
MWAKA
Mifugo
Ugonjwa
2020/2021
2021/2022
2022/2023
Kuku
Mdondo

76,416

79,672

81,416

Mbwa
Kichaa cha Mbwa

1,675

1,501

1,615

Ng’ombe
Chambavu

4,819

3,028

9,450

Ng’ombe
Homa ya mapafu

817

953

1436

Ngombe
Ugonjwa wa kutupa mimba

0

95

120

Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi.

5.2.1.5 Uvishaji wa hereni za kielektroniki

Katika zoezi la uwekaji hereni za Kielektroniki kwa mifugo mpaka wakati Serikali inasimamisha zoezi hili kupitia tamko la waziri Mkuu Bungeni, Halmashauri ya Wilaya Kakonko kupitia mzabuni ilikuwa imeshavalisha hereni kwa ng’ombe wapatao 1,030 na Mbuzi 442.

5.2.2 Uvuvi

Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ina jumla ya mabwawa ya kuchimbwa ya samaki “Digging ponds” 55.

JEDWALI 1.12: IDADI YA MABWAWA KWA MWAKA 2020/2021-2022/2023

Mwaka
2020/2021
2021/2022
2022/2023
Idadi ya mabwawa

48

55

55

Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi.

Aidha mchanganuo wa mabwawa yaliyopo ni kama inavyoonekana kwenye jedwali 1.13 hapa chini

JEDWALI 1.13: MCHANGANUO WA MABWAWA

Na.
Kata
Idadi ya Mabwawa
1.
Mugunzu

10

2.
Katanga

5

3.
Kiziguzigu

4

4.
Gwarama

17

5.
Nyabibuye

6

6.
Kasanda

7

7
Rugenge

4

8
Kanyonza

2

Jumla

55

Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi.

6.1 Sekta ya Maliasili (Misitu)

Halmashauri ya Wilaya ina misitu ya asili iliyohifadhiwa na vijiji yenye jumla ya hekta 9,598.43 kati ya hiyo misitu ya hifadhi kwa ajili ya ufugaji nyuki ina jumla ya hekta 3,142.30 na matumizi mengine hekta 6,456.13 Misitu hii ya jamii ni ya aina ya Miyombo yenye mchanganyiko wa aina mbalimbali ambazo ni Mrugwe, Mtundu, Myenzi, Mrama, Mkoyoyo, Mbanga na Mkurungu.

6.2 Sekta ya Ufugaji Nyuki

Jumla ya vikundi 40 vimeungana kuunda Ushirika wa ufugaji nyuki Buyungu (Buyungu Beekeepers Co-operative Society).  Wakala wa huduma ya misitu [TFS], Jeshi la Kujenga Taifa kambi ya Kanembwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa sasa kuna jumla ya mizinga ya kisasa 2511 na mizinga 13,690 ya asili (Mianzi) na magogo. Uhamasishaji unaendelea kwa ajili ya utengenezaji wa mizinga ya kisasa.    Katika kipindi cha mwaka 2019/2020 na 2021/2022 jumla ya kilo 33,750 za asali zilivunwa.

6.3. Ardhi.

6.3.1 Hali ya Upimaji wa Viwanja.

Katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo jumla ya viwanja 521 vilikuwa vimekamilika hatua zote za upimaji kama inavyoonekana kwenye jedwali 1.14 hapa chini

JEDWALI 1.14:  HALI YA UPIMAJI WA VIWANJA

Mwaka

Idadi

2020/2021

174

2021/2022

206

2022/2023

141

JUMLA

521

Chanzo: Idara ya Ardhi

6.3.2 Umilikishwaji na Uandaaji wa Hati Katika Mji wa Kakonko.

Kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo jumla ya hati 313 za kimila na 128 za kisheria zimetolewa kwa wanachi kama inavyoonekana kwenye Jedwali 1.15 hapa chini:-

JEDWALI 1.15 HATI ZILIZOTOLEWA KWA MWAKA 2020/2021-2022/2023 

Mwaka
Hati    zisizo    za
Hati za Kimila
Kimila
2020/2021

34

104

2021/2022

46

150

2022/2023

48

59

JUMLA

128

313

Chanzo: Kitengo cha Ardhi

6.3.3 Ukusanyaji wa kodi Ardhi.

Katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo, Wilaya imefankiwa kukusanya kodi ya ardhi kama inavyo onesha kwenye jedwali 1.16 hapa chini.

JEDWALI 1.16: UKUSANYAJI WA KODI YA ARDHI

Mwaka
Makadirio TZS
Makusanyo TZS
Makusanyo %
Isiyokusanywa TZS
2020/2021
93,000,000.00
19,668,212.00

21.15

73,331,788.00
2021/2022
40,000,000.00
23,272,716.00

58.18

16,727,284.00
2022/2023
50,000,000.00
28,105,772.00

56.21

21,894,228.00
JUMLA

183,000,000.00

 

71,046,700.00

 

38.82

 

111,953,300.00

 

Chanzo: Kitengo cha Ardhi

6.3.4 Migogoro ya Ardhi

Halmashauri imeendelea kutatua migogoro ya ardhi kila inapojitokeza ili kuhakikisha kwamba hakuna mgogoro mkubwa unaojitokeza wa kuhatarisha amani. Hata hivyo Halmashauri inaendelea na juhudi za kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji ili kuzuia kutokea kwa migogoro ya ardhi. Jedwali 1.17 hapa chini linaonyesha hali ya migogoro ya ardhi vijijini kwa mwaka 2020/2021-2022/2023


JEDWALI 1.17 IDADI YA MIGOGORO YA VIJIJI

Mwaka
Idadi     ya
Migogoro

Maelezo

2020/2021

1

Eneo la malisho na makazi – Mgogoro ulitatuliwa
2021/2022

0

Hakuna
2022/2023

0

Hakuna

Chanzo: Kitengo cha Ardhi

6.3.5 Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi

Halmashauri kwa ufadhili wa shirika la ENABEL imeandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi katika vijiji saba (7) ambavyo ni Kazilamihunda, Juhudi, Kabare, Gwarama, Rumashi, Churazo na Nyabibuye. Mpango huu umefanyika kwa ngazi zote za Vijiji, Kata na Wilaya na kupitishwa na Kamishina wa ardhi.

7.0 Sekta ya Afya

Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ina vituo 34 vya kutolea huduma za afya ambapo vituo 3 ni vituo binafsi, kama inavyoonesha kwenye jedwali 1.18 hapa chini

JEDWALI 1.18: MGAWANYO WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

MMILIKI
ZAHANATI
VITUO VYA AFYA
JUMLA
Serikali – Halmashauri

25

5

30

Serikali – JWTZ

1


1

Binafsi

2

1

3

JUMLA

28

6

34

Chanzo: Idara ya afya

 

 

HALI YA UHITAJI WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA YA AFYA

Malengo ya Serikali ni kuhakikisha kila Wilaya inakuwa na Hospitali ya Wilaya, kila Kata inakuwa na kituo cha afya na kila Kijiji kinakuwa na Zahanati ili kuwapelekea wananchi huduma kwa ukaribu Zaidi.

Mpaka kufikia Juni 30 2023, Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ina Hospitali ya Wilaya ambayo imeshaanza kutoa huduma, Kuna vituo vya afya 5 kati ya mahitaji ya vituo vya afya 13 sawa na upungufu wa asilimia 61.54 na Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ina zahanati 25 kati ya zahanati 44 sawa na upungufu wa asilimia 31.82 kama ilivyo ainishwa kwenye Jedwali 1.19 hapa chini.

JEDWALI 1.19: HALI YA UHITAJI WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA YA AFYA VYA SERIKALI


UHITAJI

VILIVYOPO

PUNGUFU

%UPUNGUFU

HOSPITALI

1

1

0

0.00

ZAHANATI

44

30

14

31.82

VITUO VYA AFYA

13

5

8

61.54

Chanzo: Idara ya Afya

7.1 Mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU).

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yamekuwa yakiendelea ambapo kasi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI imepungua kutoka asilimia 2.7 kwa mwaka 2021/2022 mpaka asilimia 2.02 kwa mwaka 2022/2023. Hali ya mapambano dhidi ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni kama inavyoonekana kwenye Jedwali 1.20 hapa chini;

JEDWALI 1.20: HALI YA MAPAMBANO DHIDI YA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI

MWAKA

2021/2022

2022/2023

Watu wanaoishi na VVU (HIV positivity rate)

2.7%

2.02%

Vituo  vya  kutolea  huduma  ya  UKIMWI  (refilling center)

14

14

Vituo  vya  matunzo  na  tiba  (care  and  treatment center)

4

4

Kituo   cha   matunzo   na   tiba   -TRC   kambi   yawakimbizi Mtendeli

1

0

Chanzo: Idara ya Afya

7.2 Uthibiti wa ugonjwa wa Malaria.

Kwa mwaka 2022/2023 kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa Malaria imeongeza kutoka asilimia 33 ya mwaka 2021/2022 hadi asilimia 33.2. Sababu kuu ya ongezeko hilo ni kuisha kwa mradi wa mdau wa unyunyuziaji wa dawa ya ukoko majumbani pamoja na unyunyuziaji katika vyanzo vya mazalia ya Mbu. Halmashauri bado inaendelea na jitihada za kutafuta mdau mwingine pamoja na kutafuta vyanzo vingine vya fedha ili kuweza kuendeleza zoezi la unyunyuziaji na kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa Malaria.

Kiwango cha maambukizi ya Malaria baina ya wagonjwa wanaofika vituo vya afya ni kama inavyoonesha kwenye jedwali 1.21 hapa chini:

JEDWALI 1.21 KIWANGO CHA MAAMBUKIZI YA MALARIA

Mwaka
Kiwango   cha   maambukizi   ya   malaria   kwa   wagonjwa
wanoafika katika vituo vya kutolea huduma za Afya.
2020/2021

28%

2021/2022

33%

2022/2023

33.2%

Chanzo: Idara ya Afya

7.3 Huduma za afya ya uzazi na mtoto

Huduma ya mama na mtoto inatolewa katika vituo 26 vya kutolea huduma za afya. Kwa kipindi cha miaka mitatu vifo vya akina mama vimepungua na hili ni juhudi za serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama UMATI, AMREF, Marie Stoppes na THPS kupambana kuhakikisha Halmashauri inamaliza vifo vyote vya akina mama wajawazito

Vifo vya mama wajawazito vimepungua kutoka vifo 3 kwa mwaka 2021/2022 mpaka kifo 1 kwa mwaka 2022/2023. Hali ya vifo vya akina mama wajawazito ni kama inavyoonekana kwenye Jedwali 1.22 hapa chini.

JEDWALI 1.23: HALI YA VIFO VYA AKINA MAMA WAJAWAZITO

Mwaka
Idadi ya vifo vya akina mama
2020/2021

7

2021/2022

3

2022/2023

1

Chanzo: Idara ya Afya

7.4 CHF iliyoboreshwa.

Halmashauri ina wanachama 3503 wa CHF iliyoboreshwa ambayo ni sawa na 11.1. Kuna baadhi ya changamoto zinapunguza kasi ya uandikishaji wa CHF changamoto kama kutokulipwa kwa wakati madai ya vituo na zahanati, bei za vipimo, dawa na baadhi ya huduma zingine kutokuwekwa wazi, pia mfumo wa madai kutolipa fomu zote za madai kama madai yalivyo.

7.5 Hali ya Upatikanaji wa Dawa na Vifaa Tiba

Hali ya upatikanaji wa dawa muhimu ni 87%. Pamoja na upatikanaji huo, maombi ya dawa yanapowasilishwa huletwa dawa baadhi tu na wakati mwingine sio kwa kiwango kilichoagizwa. Pamoja na hayo Halmashauri inaendelea kufanya mawasiliano ya karibu na MSHITIRI ili kusaidia kuleta kwa wakati dawa ambazo hazipatikani kwenye Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD).

7.6 Matibabu ya wazee

Kwa kipindi cha Miaka mitatu 2020/2021- 2022/2023Jumla ya wazee 6,073 wametambuliwa katika kata zote 13 za Wilaya 3,066 kati yao wakiwa wanaume na 3,007 wakiwa wanawake. Pia kuna jumla ya mabaraza ya wazee 58 ambapo baraza 1 ni nganzi ya halmashauri, mabaraza 13 kwa kata zote na mabaraza 44 kwa vijiji vyote. Halmashauri ya Wilaya katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo imetoa huduma za afya kwa wazee bure kulingana na sera na miongozo ya serikali kama inavyoonekana kwenye jedwali 1.24 hapa chini.

JEDWALI 1.24 WAZEE WALIOTAMBULIWA

Mwaka

Me

Ke

Jumla

2020/2021

2,143

2,006

4,149

2021/2022

577

623

1,200

2022/2023

346

378

724

Jumla

3,066

3,007

6,073

Chanzo: Idara ya Afya

7.7 Uboreshaji wa miundombinu katika vituo vya kutolea huduma za Afya. 

Kwa kipindi cha miaka mitatu 2020/2021- 2022/2023 Halmashauri ya wilaya ya Kakonko ilitengewa kiasi cha Shilingi 4,871,401,494.00 kutoka Serikali Kuu, Mapato ya ndani ya Halmashauri na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa ajili ya kuboresha miundombinu mbalimbali ya Afya katika Hospitali ya Wilaya, Zahanati na Vituo vya Afya vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.Katika fedha hizo kiasi cha Shilingi 1,342,000,000.00 sawa na asilimia 27.5 kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2020/2021, kiasi cha shilingi 2,211,000,000.00 sawa na asilimia 45.4 kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na kiasi cha shilingi 1,318,401,494.00 sawa na asilimia 27.1 kilitengwa kwa mwaka 2022/2023.

JEDWALI 1.25: UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

Na
Aina ya mradi
Chanzo cha fedha
Mwaka wa Mapokezi ya fedha
hatua ya utekelezaji
 Kiasi cha Fedha kilichopokelewaTsh 

1

ujenzi wa jengo la utawala, jengo la kufulia, pharmacy, jengo la mionzi, jengo la Maternity Hospitali ya Wilaya
SERIKALI KUU
2020/2021
ujenzi umekamilika

1,000,000,000.00

2

Ukarabati wa zahanati ya kinonko
SERIKALI KUU
2020/2021
ukarabati umekamilika

50,000,000.00

3

Ukarabati wa zahanati ya bukiliro
SERIKALI KUU
2020/2021
ukarabati umekamilika

50,000,000.00

4

Ukarabati wa zahanati ya Kiduduye
SERIKALI KUU
2020/2021
ukarabati umekamilika

50,000,000.00

5

ujenzi wa zahanati ya chilambo
WORLD VISION
2020/2021
ujenzi umekamilika

192,000,000.00

 

jumla ndogo 2020/2021
 
 
 

1,342,000,000.00

6

Ujenzi wa kituo cha afya Mugunzu
TOZO (SERIKALI KUU)
2021/2022
Ujenzi bado unaendelea

500,000,000.00

7

ujenzi wa jengo la EMD Hospitali ya Wilaya
SERIKALI KUU
2021/2022
ujenzi umekamilika

300,000,000.00

8

ujenzi wa nyumba moja ya watumishi wa Hospitali ya Wilaya
SERIKALI KUU
2021/2022
ujenzi umekamilika

90,000,000.00

9

Umaliziaji wa Zahanati ya Rusenga
SERIKALI KUU
2021/2022
Kuweka vigae na dari

50,000,000.00

10

Umaliziaji wa zahanati ya Luhuru
SERIKALI KUU
2021/2022
uko hatua ya plasta

50,000,000.00

11

ukarabati wa zahanati ya Rumashi
SERIKALI KUU
2021/2022
ukarabati umekamilika

50,000,000.00

12

Ujenzi wa Wodi ya kina mama zahanati ya Gwarama
UNFPA
2021/2022
ujenzi umekamilika

75,000,000.00

13

Ujenzi wa Kituo cha afya Nyakiyobe
SERIKALI KUU
2021/2022
OPD na maabara zimekamilika maternity complex umaliziaji vyooni

500,000,000.00

14

Ujenzi wa Wodi ya kina mama zahanati ya nyamtukuza
WORLD VISION
2021/2022
ujenzi umekamilika

85,000,000.00

15

Ujenzi wa zahanati ya churazo
WORLD VISION
2021/2022
ujenzi umekamilika

200,500,000.00

16

Ujenzi wa Zahanati ya ilabiro
WORLD VISION
2021/2022
ujenzi umekamilika

200,500,000.00

17

Ujenzi wa zahanati ya Kihomoka (mapato ya ndani)
MAPATO YA NDANI
2021/2022
ujenzi umekamilika

55,000,000.00

18

ujenzi wa zahanati ya Njoomlole (mapato ya ndani)
MAPATO YA NDANI
2021/2022
ujenzi umekamilika

55,000,000.00

 

jumla ndogo 2021/2022
 
 
 

2,211,000,000.00

19

Umaliziaji wa Zahanati ya Luhuru
SERIKALI KUU
2022/2023
Upo katika hatua ya kupiga plasta

50,000,000.00

20

Umaliziaji wa zahanati ya Rusenga
SERIKALI KUU
2022/2023
Kuweka vigae na dari

50,000,000.00

21

Ujenzi wa wodi tatu za baba, mama na mtoto
SERIKALI KUU
2022/2023
uwekaji wa terazo

750,000,000.00

22

ujenzi wa nyumba za watumishi 2in1 zahanati ya Chilambo
WORLD VISION
2022/2023
ujenzi uko katika hatua ya upauaji

246,936,262.00

23

ujenzi wa nyumba za watumishi 2in1 zahanati ya Churazo
WORLD VISION
2022/2023
ujenzi uko katika hatua ya upauaji

221,465,232.00

 
jumla ndogo 2022/2023
 
 
 

1,318,401,494.00

 
JUMLA KUU
 
 
 

4,871,401,494.00

Chanzo: Idara ya Afya

(C) UJENZI WA MATUNDU YA VYOO KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

Pia katika mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2022/2023 Halmashauri kupitia mradi wa Program ya Maji na Usafi wa Mazingira Afya unaofadhiliwa na Benki ya Dunia Vimejengwa vyoo na kuweka mifumo ya maji katika vituo vya kutolea huduma za afya 16 kwa jumla ya gharama ya Shilingi 311,608,000.00 ambapo kiasi cha shilingi 176,000,000.00 kilitumika kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kiasi cha shilingi    135,608,000.00 Kilitumika kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Ujenzi wa vyoo katika vituo vyote 16 umekamilika. Mchanganuo wa matundu ya vyoo yaliyotengenezwa ni kama ilivyo kwenye jedwali 1.26 hapa chini.

JEDWALI 1.26 MIUNDOMBINU YA CHOO KUPITIA WASH

Huduma
Hatua
ukamilishaji
Jumla Sh.
Vituo vya Afya @ 22,000,000.00 kakonko,
Gwanumpu, Nyanzige, Kiduduye, Kazilamihunda, Katanga,  Muhange, Nyabibuye, Gwarama, Kasanda, Nyamtukuza na Kabingo

100%

   242,000,000.00

Vituo vya Afya @ 17,408,000.00 Kasongati, Kiga na
Bukirilo

100%

52,224,000.00

Kituo cha Afya Rumashi

100%

17,384,000.00

JUMLA
311,608,000.00

Chanzo: Idara ya Afya

 

 


 

8.0 Sekta ya Elimu

8.1 Elimu ya Awali na Msingi

Halmashauri wa Wilaya ya Kakonko ina jumla ya shule za Msingi 67 ambapo kati ya hizo shule za Serikali ni 66 na shule binafsi ni 1. Shule zote hizi zinajumuisha wanafunzi wa Elimu ya Awali hadi darasa la VII. Mpaka kufikia Juni 2023 Halmashauri ina Jumla ya wanafunzi 50,911 kuanzia elimu ya awali hadi darasa la saba ambapo kati yao wavulana ni wanafunzi 25,355 sawa na asilimia 49.8 na wasichana ni 25,556 sawa na asilimia 50.2. Aidha idadi ya wanafunzi waliopo shule za Serikali ni 50,776 sawa na asilimia 99.73 na wanafunzi wa shule binafsi ni 135 sawa na asilimia 0.27

Katika shule za Msingi za serikali Kuna jumla ya walimu 578 kati ya mahitaji ya walimu 1189 na hivyo kuna upungufu wa walimu 611. Aidha kwa upande wa elimu ya awali kuna walimu 14 kati ya mahitaji ya walimu 224 hivyo kufanya upungufu kuwa walimu 210.

8.1.1 Hali ya uandikishaji wa wanafunzi

Kwa mwaka wa masomo wa 2023 wanafunzi 6460 wa Elimu ya Awali waliandikishwa kati ya 6123 waliotarajiwa sawa na asilimia 106 ya uandikishaji. Aidha kwa elimu ya Msingi, kwa mwaka wa masomo 2023 wanafunzi 6781 wa elimu ya masingi nwaliandikishwa kati ya wanafunzi 6,054 waliotarajiwa. Hali ya uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali imeongezeka kutoka asilimia 46 ya uandikishaji kwa mwaka wa masomo 2022 hadi asilimia 106 ya uandikishaji kwa mwaka 2023. Jedwali lifuatalo hapa chini linaonesha hali ya uandikishaji wa Elimu Awali na Msingi kwa mwaka wa masomo 2021-2023. Mchanganuo wa uandikishaji ni kama ilivyo kwenye jedwali 1.27 hapa chini

JEDWALI 1.27: HALI YA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI

MWAKA

HALI YA UANDIKISHAJI

ELIMU YA AWALI

ELIMU MSINGI

MALENGO

Wav
Was
JUMLA
% ya uandikishaji
MALENGO
wav
was
JUMLA
%

2021

5937

1546

1565

3111

52

         5,175

3012

3014

6026

  116

2022

7350

1685

1696

3381

46

         6,090

3486

3335

6821

  112

2023

6123

3132

3328

6460

106

         6,054

3403

3378

6781

  112

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi.

8.1.2 MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE (SFNA) NA DARASA LA SABA (PSLE) 

Hali ya ufaulu katika mtihani wa upimaji wa darasa la nne (SFNA) imeshuka kutoka asilimia 78.16 mwaka 2021 hadi asilimia 65.15 mwaka 2022, aidha hali ya ufaulu wa mtihani wa kuhitimu darasa la saba (PSLE) imeshuka kutoka asilimia 73.11 kwa mwaka 2021 hadi asilimia 65 kwa mwaka 2022. Sababu kuu zilizosababisha ufaulu kushuka ni pamoja na ongezeko la Utoro wa wanafunzi ambapo Halmashuri imetoa maelekezo kuanzia kwa walimu wakuu, watendaji wa vijiji, Maafisa Elimu kata, watendaji wa kata, makatibu tawala na wasimamizi wa elimu ngazi ya Halmashauri kuhakikisha wanafuatilia suala la utoro kwa ukaribu na kutoa taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri. Hali hii imepunguza utoro wa wanafunzi kwa kiasi kikubwa na matarajio kwa mitihani ijayo ni kuongezeka ufaulu.

Sababu nyingine ni Wazazi kuwa na mwamko mdogo katika masuala ya kielimu mfano kuwakataza watoto wao wasifanye vizuri mitihani ya Taifa ili wasigharamie mahitaji pindi wanapokuwa wamefaulu na kutakiwa kujiunga na kidato cha Kwanza.  Wasimamizi wa elimu ngazi ya Halmashauri na wilaya wamekuwa wakitoa elimu kwa wazazi na jamii juu ya umuhimu wa elimu kupitia mikutano na vikao mbalimbali, wazazi ambao wamebainika kuwakataza Watoto wao wasifanye vizuri kuripotiwa kwa watendaji wa vijiji na kuwataka wajieleze kwa maandishi juu ya kutowakataza watoto wao wasifanye vizuri kwenye mitihani ya Taifa. Pia, imeanzishwa programmu ya ushirikiano wa walimu na wazazi (UWAWA) katika kusimamia na kushiriki katika kuleta maendeleo ya shule ikiwa ni Pamoja na kuinua ufaulu wa wanafunzi kwa mitihani ya Taifa. Upungufu wa walimu nao umechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa ufaulu ila matarajio kwa mitihani ijayo ni kuongezeka ufaulu kwani Serikali imeendelea kuajiri walimu wapya katika kukabiliana na changamoto hii ya upungufu wa walimu shuleni.

Katika Mtihani wa Upimaji wa Darasa la Nne (SFNA) na Mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi (PSLE) kwa miaka mitatu mfululizo ufaulu ulikuwa kama inavyoonekana katika jedwali 1.28 lifuatalo hapa chini.

JEDWALI 1.28: HALI YA UFAULU SFNA NA PSLE

MWAKA

WALIOFANYA MITIHANI

WALIOFAULU SFNA

WALIOFANYA MTIHANI

WALIOFAULU PSLE

WAV
WAS
JUMLA
%UFAULU
WAV
WAS
JUMLA
%UFAULU

2020

5759

2480

2452

4932

        85.64
   2,768.00

1138

1014

2152

        77.75

2021

5545

2043

2291

4334

        78.16
   3,782.00

1442

1323

2765

        73.11

2022

         6446

1967

237

4339

        65.15
         4,694

1655

1539

3194

65

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi.

8.1.3 Fedha za Elimu bila malipo

Katika kipindi kuanzia mwaka 2020/2021 hadi 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imepokea jumla ya shilingi 1,532,405,576.71Kwa ajili ya uendeshaji wa shule kwa shule za msingi 59 kati ya 66 zilizopo Wilayani kama ifuatavyo kwenye jedwali 1.29.

JEDWALI 1.29 MAPOKEZI YA FEDHA ZA ELIMU BILA MALIPO

Na
MWAKA
KIASI KILICHOKELEWA (TZS).
1
2020/2021

438,743,958

2
2021/2022

516,526,023

3
2022/2023

577,135,595.71


JUMLA

1,532,405,576.71

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi.

8.1.4 Ujenzi wa miundombinu

Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 – 2022/2023 kupitia fedha zinazotolewa na serikali pamoja na wadau wa maendeleo, Halmashauri imetekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu kama ilivyo kwenye jedwali 1.30 na 1.31 hapa chini;-

JEDWALI 1.30: UJENZI WA MIUNDOMBINU KWA MWAKA 2021/2022-2022/2023

Na

MWAKA

Ujenzi vyumba vya madarasa

Ukarabati vyumba vya madarasa shule kongwe

Matundu ya vyoo

Ujenzi wa nyumba za walimu




1

2020/2021

19

6

126

0


2

2021/2022

23

10

156

0


3

2022/2023

11

7

188

7


Chanzo: Idara ya Elimu Msingi.

Ujenzi wa Miundombinu ya Darasa kupitia mradi wa BOOST

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imepokea kiasi cha shilingi   1,457,800,000.00 kupitia Mradi wa BOOST kwa ajili ya kujenga miundombinu mipya ya elimu msingi na awali ambapo kiasi cha shilingi 723,000,000.00 sawa na asilimia 49.60 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa shule 2 mpya , kiasi cha shilingi 520,000,000.00 sawa na asilimia 35.67 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 20 vya madarasa, kiasi cha shilingi 71,800,000.00 sawa na asilimia 4.93 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 2 ya mfano elimu ya awali, shilingi  33,000,000.00 sawa na asilimia 2.26 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa vyoo matundu 15 na kiasi cha Shilingi 110,000,000.00 sawa na asilimia 7.55 ikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba ya walimu 2in1. Mchanganuo ni kama ulivyo kwenye Jedwali 1.31 hapa chini;

JEDWALI 1.31: UJENZI WA MIUNDOMBINU YA DARASA KUPITIA MRADI WA    BOOST

Na 
 JINA LA SHULE 
 MRADI 
 IDADI 
 KIASI 
 JUMLA 
     1.00
 KAZILAMIHUNDA  
 Ujenzi wa Shule Mpya

          1.00

   361,500,000.00

     361,500,000.00

     2.00
 NYAMTUKUZA  
 Ujenzi wa Shule Mpya

          1.00

   361,500,000.00

     361,500,000.00

 
 
 JUMLA NDOGO 

          2.00 

 

     723,000,000.00 

     3.00
 GWARAMA  
 Ujenzi wa vyumba vya madarasa

          4.00

     26,000,000.00

     104,000,000.00

     4.00
 BUKIRILO  
 Ujenzi wa vyumba vya madarasa

          4.00

     26,000,000.00

     104,000,000.00

     5.00
 KIGARAMA  
 Ujenzi wa vyumba vya madarasa

          4.00

     26,000,000.00

     104,000,000.00

     6.00
 Nyamwirongwe
 Ujenzi wa vyumba vya madarasa

          4.00

     26,000,000.00

     104,000,000.00

     7.00
 Kavungwe
 Ujenzi wa vyumba vya madarasa

          4.00

     26,000,000.00

     104,000,000.00

 
 
 JUMLA NDOGO 

        20.00 

 

     520,000,000.00 

     8.00
 GWARAMA  
 Ujenzi wa madarasa mfano elimu ya awali

          2.00

     35,900,000.00

        71,800,000.00

 
 
 JUMLA NDOGO 

          2.00 

 

        71,800,000.00 

     9.00
 GWARAMA  
 Ujenzi wa matundu ya vyoo

          3.00

       2,200,000.00

          6,600,000.00

   10.00
 BUKIRILO  
 Ujenzi wa matundu ya vyoo

          3.00

       2,200,000.00

          6,600,000.00

   11.00
 KIGARAMA  
 Ujenzi wa matundu ya vyoo

          3.00

       2,200,000.00

          6,600,000.00

   12.00
 Nyamwirongwe
 Ujenzi wa matundu ya vyoo

          3.00

       2,200,000.00

          6,600,000.00

   13.00
 Kavungwe
 Ujenzi wa matundu ya vyoo

          3.00

       2,200,000.00

          6,600,000.00

 
 
 JUMLA NDOGO 

        15.00 

 

        33,000,000.00 

   14.00
 Nyakivyiru
 Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu

          1.00

   110,000,000.00

     110,000,000.00

 
 
 

            1.00 

 

         110,000,000.00 

 JUMLA KUU 

 
 
  1,457,800,000.00 

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

Jedwali 1.32 hapa chini linaonesha hali ya Miundombinu na samani katika shule za msingi kwa ujumla; -

JEDWALI 1.32 HALI YA MIUNDOMBINU NA SAMANI KATIKA SHULE ZA MSINGI

AINA YA MIUNDOMBINU
MAHITAJI
ILIYOPO
UPUNGUFU
OFISI YA WALIMU

170

98

72

MADARASA

1205

580

625

NYUMBA ZA WALIMU

1157

209

948

VYOO

2297

934

1363

MADAWATI

16142

12125

4017

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi.

8.2.0 Elimu ya Sekondari.

Kwa Mwaka 2022/2023 Halmashauri ina jumla ya shule 20 za sekondari, kati ya hizo 16 ni za Serikali na 4 zisizo za Serikali zenye jumla ya wanafunzi 9,461 kati ya hao wavulana ni 4943 na wasichana 4518. Halmashauri ina shule moja ya kidato cha kwanza hadi cha sita ambayo ni Kakonko sekondari na shule 1 ya kidato cha tano na sita inayotarajia kupokea wanafunzi mwezi Julai 2023 ambayo ni shule ya sekondari Amani Mtendeli.  Halmashauri ina jumla ya walimu 186 kati ya 280 wanaohitajika hivyo kuwa na upungufu wa walimu 94 kwa shule za Serikali sawa na asilimia 33.57. Kati ya walimu waliopo wanaofundisha masomo ya sayansi na hisabati ni 93 na Sanaa ni 93. Vile vile Halmashauri ina wataalam wa maabara 3 kati ya 16 ya uhitaji hali inayopelekea upungufu wa wataalam 13 wa maabara.

8.2.1 Hali ya Uandikishaji

Halmashauri inatekeleza sera ya elimu bila malipo kwa upande wa sekondari kwa kuhakikisha kila mtoto mwenye sifa anadahiliwa kidato cha kwanza. Kwa mwaka 2023 Halmashauri imedahili wanafunzi 3,187 kati ya 3,198 waliolengwa sawa na asilimia 99.7. Hali ya uandikishaji ni kama ilivyo kwenye jedwali 1.33 hapa chini.

JEDWALI 1.33: HALI YA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI SHULE ZA SEKONDARI

Mwaka
Maoteo
Walioandikishwa
Uandikishaji %
2020/2021

1834

1670

91.05

2021/2022

2,134

1,941

91

2022/2023

3198

3187

99.7

Chanzo: Elimu Sekondari

8.2.2 Hali ya ufaulu

Hali ya ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha pili umepungua kutoka asilimia 90 mwaka 2021 hadi asilimia 86.8 mwaka 2022. Kwa upande wa kidato cha nne ufaulu umeshuka kutoka 88.7% mwaka 2021 hadi 85% kwa mwaka 2022. Aidha ufaulu kwa kidato cha sita umeongezeka kutoka 99% mwaka 2021 hadi 100% mwaka 2022. Sababu kuu ya kushuka kwa ufaulu wa mitihani ya kidato cha pili na kidato cha nne ni ongezeka la wanafunzi wanaotoroka kipindi cha masomo kuja kufanya mitihani kipindi cha mitihani. Kutokana na utafiti uliofanywa na Idara za Elimu Msingi na Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko mwaka 2022 matokeo ya utafiti yalionyesha ongezeko la utoro linasababishwa na ukosefu wa chakula cha kutosha shule na ubovu wa miundombinu ya kujifunzia na ujifunzaji. Aidha Halmashauri imeshachukua hatua mbalimbali zitakazosaidia kupunguza utoro ili hali ya ufaulu iweze kupanda ikiwa ni pamoja na kuhakikisha uwepo wa vyakula shuleni kuboresha miundombinu na kuwachukulia hatua kali wale wanaowasababishia wanafunzi kutoroka au kuacha shule. Sababu nyingine ni uhaba wa walimu ambapo Serikali imeendelea kuajiri walimu hivyo utatuzi wa changamoto hii itasaidia kwa kiasi kikubwa ufaulu kuongezeka. Mchanganuo wa ufaulu ni kama jedwali 1.34 linavyobainisha hapa chini:-

JEDWALI 1.34: HALI YA UFAULU WA MITIHANI KWA KIDATO CHA PILI, KIDATO CHA NNE NA KIDATO CHA SITA

MWAKA
KIDATO
WALIOFANYA
WASIOFANYA
MADARAJA YA UFAULU
%    YA
UFAUL U
WV
WS
JML
WV
WS
JML
I
II
III
IV
0
JML
2020
II

814

819

1633

65

38

103

146

137

225

965

156

1633

90.2

IV

562

526

1088

3

10

13

68

169

179

521

151

1088

86

VI

2

31

33

0

0

0

10

21

2

0

0

33

100

2021
II

784

717

1501

49

27

76

141

164

201

842

157

1501

90

IV

646

571

1217

7

7

14

48

194

202

636

137

1217

88.7

VI

142

72

214

0

0

0

34

116

63

1

0

214

100

2022
II

872

762

1634

29

29

58

73

110

206

1007

234

1630

86.8

IV

702

674

1376

5

10

15

52

133

211

762

203

1361

85

Chanzo: Idara ya Elimu Sekondari.

8.2.3 Hali ya miundombinu katika shule za sekondari

Kwa mwaka 2023 kuna miundombinu ambayo ina upungufu kutokana na mahitaji na kuna miundombinu mingine ina ziada ukilinganisha na mahitaji. Hali ya miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika shule za sekondari ni kama ifuatavyo kwenye jedwali 1.35 hapa chini

JEDWALI 1.35 HALI YA MIUNDOMBINU KATIKA SHULE ZA SEKONDARI

AINA YA MIUNDOMBINU
MAHITAJI
ILIYOPO
UPUNGUFU/ZIADA
% UPUNGUFU/ZIADA
MAABARA

45

17

28

62.22

MADARASA

204

252

48

23.53

NYUMBA ZA WALIMU

187

70

117

62.57

VYOO

394

243

151

38.32

MAJENGO YA UTAWALA

16

10

6

37.50

HOSTELI

69

21

48

69.57

MEZA

8350

9324

974

11.66

VITI

8350

9323

973

11.65

Chanzo: Idara ya Elimu Sekondari.

 

8.2.4 Mapokezi ya fedha za elimu bila malipo kwa sekondari.

Katika kipindi kuanzia mwaka 2020/2021 hadi mwezi Juni 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imepokea jumla ya shilingi 1,479,199,249 za Elimu Bila Malipo kwa shule kwa shule zote 12 za sekondari kama ifuatavyo kwenye jedwali 1.36 hapa chini:

JEDWALI 1.36 MAPOKEZI YA FEDHA ZA ELIMU BILA MALIPO

Na
MWAKA
KIASI KILICHOPOKELEWA (Shilingi).
1
2020/2021

401,132,422

2
2021/2022

476,833,333

3
2022/2023

601,233,494.07


JUMLA

1,479,199,249

Chanzo: Idara ya Elimu Sekondari.

9.0 Uwezeshaji Wananchi kiuchumi

9.1. Sekta ya Maendeleo ya Jamii           

9.2 Uanzishaji wa vikundi vya Kiuchumi

Kwa kipindi cha mwaka 2020/2021- 2022/2023. Halmashauri imefanikiwa kusajili vikundi 242 vyenye jumla ya wanachama 2338 ambapo kati yao wanachama 628 sawa na asilimia 26.86 ni wanaume na wanachama 1710 sawa na asilimia 73.14 ni wanawake. Katika kipindi hicho idara ya Maendeleo ya Jamii imetoa mafunzo ya kuweka na kukopa kwa wanachama 1,145 ambapo kati yao wanaume ni 405 na wanawake ni 740


 

9.3 Utoaji wa Mikopo inayotokana na tengo la 10% ya Mapato ya ndani

Kwa kipindi cha miaka mitatu 2020/2021 – 2022/2023 jumla ya vikundi 64 vya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu viliwezeshwa jumla ya shilingi 425,724,770 kama ifuatavyo kwenye jedwali 1.37 hapa chini: -

JEDWALI 1.37: UKOPESHAJI KWA VIKUNDI

Mwaka
Idadi ya Vikundi
Kiasi TZS
2020/2021

18

99,484,000

        99,484,000

        99,484,000

2021/2022

25

164,240,770

2022/2023

21

162,000,000

Jumla

64

425,724,770

 

Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

9.4 Kiasi cha fedha kilichopokelewa TASAF III Awamu ya pili

Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2022/2023 jumla ya shilingi 5,135,280,085.00 zilipokelewa ikiwa ni fedha kwa ajili ya Walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikini. Jedwali 1.38 hapa chini linaonesha mapokezi kila mwaka.

JEDWALI 1.38: MAPOKEZI YA FEDHA ZA TASAF 

Mwaka
Mapokezi
2020/2021

1,395,313,920.00

2021/2022

2,272,600,860.00

2022/2023

1,467,365,305.00

JUMLA

5,135,280,085.00

 

Chanzo: Ofisi ya TASAF Wilaya

NB;Unaweza kupakua nakala ya wasifu wa Halmashauri hapa chini;

4. wasifu mfupi wa Halmashauri3.pdf

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa