• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Usafishaji Na Mazingira

TAARIFA YA HALI YA USAFI NA HIFADHI YA MAZINGIRA WILAYANI KAKONKO KATIKA ROBO YA PILI 2016/2017

USAFI WA MAZINGIRA NA MAENEO YA BIASHARA

Ukaguzi wa nyumba za biashara

Ukaguzi wa nyumba za bishara umefanyika katika kata ya Kasanda, Kakonko Katanga na nyabibuye na

Biashara zilizokaguliwa ni kama ifuatavyo:

  • Migahawa - Jumla ya migahawa 21 ilikaguliwa na kupewa maelekezo ya mdomo na maandishi.
  • Baa na vilabu.5 vimekaguliwa na kupewa maelekezo ya kuzingatia usafi
  • Mashine za kusaga 8,
  • Bucha 3,
  • Maduka ya vyakula 11 na maduka ya dawa 3.
  • Machinjio moja ambayo ukaguzi wa TFDA uliifunga na kushauri ijengwe machinjio nyingine inayolingana na hadhi ya Wilaya.

USAFI WA MAZINGIRA 

Ufuatiliaji na ukaguzi wa mazingira umefanyika katika kata ya Kasanda, Katanga Kakonko mjini Gwanumpu na Rugenge. Kazi hizi zimefanywa na kamati za mazingira za vijiji. Katika mji wa Kakonko ukaguzi unafanyika kila siku ya Alhamisi ambapo kila mtaalam wa afya huenda kwenye kitongoji anachokilea kuhamasisha usafi na kufanya ukaguzi.

HATUA ZILIZOCHUKULIWA

Baada ya ukaguzi hatua zilizochukuliwa katika ngazi za vijiji zilikuwa ni kuwaita wale ambao hawana vyoo na wenye vyoo vibovu na wlitozwa faini kama ifuatavyo;

Kata ya Rugenge

  • Kijiji cha Kikulazo watu 24 waliitwa na kutozwa faini y ash 5,000 kila mmoja  na kuagizwa kukamilisha vyoo ifikapo tarehe 18/11/2016
  • Kijiji cha kasongati watu 19 walitozwa faini lakini wote waligoma  kutoa faini na kuamuliwa kupelekwa baraza la kata
  • Kijiji cha kiga hatua zilichukuliwa kwa kuwaita ofisi ya kijiji na kuwatoza faini lakini hakuna aliyetoa faini uongozi wa kijiji ukaamua kuwapeleka Baraza la kata.

Kata ya Kasanda

  • KIJIJI cha Kazilamihunda waliokutwa hawana choo walikuwa 11 waliotozwa faini  ni watu 6 kiasi cha sh 30,000/=
  • Kijiji cha juhudi waliokutwa hawana choo ni 10 walotozwa faini  ni 4 kiasi cha sh 15,000/=
  • Kijiji cha Kewe waliokutwa hawana vyoo ni 90 waliotozwa faini ni 41 kiasi cha sh 358,000/=.
  • Kijiji cha Kasanda waliokutwa hawana choo walikuwa 114 waliotozwa faini 20 kiasi cha sh 200,000/=
  • Kijiji cha Nkuba waliokutwa hawana choo ni 70 waliotozwa faini ni 6 kiasi cha sh 60,000/=
  • Kijiji cha Chilambo waliokutwa hawana choo walikuwa 64 uongozi wa Kijiji haujachukua hatua yoyote.mtendaji wa Kata ameagizwa kufuatilia uongozi wa kijiji hiki kujua kulikoni.

Mji wa Kakonko

Katika mji wa kakonko kazi ilifanyika katika vitongoji kama ifuatavyo

  • Kitongoji cha msufini Waliokutwa hawana vyoo ni 4 ambao hawana vyombo vya taka taka walikuwa 21 wenye vyoo vibovuwalikuwa 12.
  • Kitongoji cha Kumuyumpu waliokutwa hawana vyoo ni 1 ambao hawana vyombo vya kuhifadhia taka walikuwa  0 wenye vyoo vibovu walikuwa 44
  • Kitongoji cha Kanyomvi waliokutwa hawana vyoo walikuwa 16 ambao hawana vyombo vya kuhifadhia taka walikuwa 29 wenye vyoo vibovu walikuwa 13
  • Kitongoji cha Migombani waliokutwa hawana choo walikuwa ni 3 wasio na vyombo vya kuhifadhi taka 22 na wenye vyoo vibovu walikuwa 20
  • Kitongoji cha waliokutwa hawana choo walikuwa 0 wasiona vyombo vya kuhifadhia taka walikuwa 18 na wenye vyoo vibovu walikuwa 41
  • Kitongoji cha Kanyaga waliokutwa hawana choo walikuwa 0 ambao hawana vyombo vya kuhifadhia taka 15 na wenye vyoo vibovu walikuwa 20.

Katika mji wa Kakonko majina 147 ya wale wote waliokutwa ni wachafu yako ofisi ya mwanasheria yanafanyiwa upembuzi wa kisheria ili hatua muafaka zichukuliwe hasa ukizingatia kwamba sheria ndogo za halmashauri bado hazijaruhusiwa kutumika.

Aidha maafisa wa afya ambao walikabidhiwa kufanya ukaguzi wa afya katika vitongoji na hawajakamilisha kazi yao wameandikiwa barua ya kujieleza ni kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya msingi.

HALI HALISI KATIKA MAENEO YALIYOKAGULIWA ni kama inavyoonekena katika jedwali hapa linalofuata

Na
Jina la kata
Kaya zilizokaguliwa
Kaya zenye vyoo bora
Kaya zenye vyoo vya asili
Kaya zisizo na vyoo
Kaya zenye vifaa vya taka/mashimo ya taka
Kaya zenye vichanja

Kakonko mjini
451
269
161
21
327
131

kasanda
3,033
311
2363
359
2,087
2,417

Rugenge
1,677
24
1,388
75
1,180
1,411

jumla
5,161
604
3,912
455
3,594
3,959

UTEKELEZAJI WA KUFANYA USAFI KILA JUMAMOSI YA MWISHO WA MWEZI.

Usafi umekuwa ukifanywa na wananchi katika maeneo yao. aidha viongozi na watumishi wa serikali katika jumamosi ya mwisho wa mwezi wa 10 wakiongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kakonko walifanya usafi katika viwanja vya Parokia ya kanisa Katoliki kakonko mjini na kuzibua mifereji ya maji ya mvua katika barabara zenye urefu wa mita 500.  Jumamosi ya mwisho wa mwezi Novemba  walifanya usafi katika eneo la wazi la Kakonko mjini ambako kuna kizimba cha kuhifadhia taka karibu na kanisa la Anglikana.

Jumamosi ya mwisho wa mwezi Dec walifanya usafi katika maeneo ya Ofisi za Halmashauri hasa kazi kubwa ilikuwa kufyeka nyasi na kufagia maeneo yote ya ofisai za Halmashauri. Mahudhurio katika utekelezaji yamekuwa ya kutosha wanhudhuria watumishi 45 hadi 50 kati ya 60 ambao wako makao akuu ya Halmashauri.

Kwa wananchi wa kawaida siku hiyo ni siku ya soko kuu ushiriki wao ni mdogo sana.

 

Uzoaji wa takataka 

Idara ya usafi na mazingira imeanisha eneo muafaka ambalo litakuwa dampo kuu la mji wa kakonko .eneo hilo liko kilomita 8.5 kutoka kakonko mjini kulekea mashariki na liko kilomita 6 toka katika mto wa muhwazi katika kijiji cha itumbiko.

Taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja upimaji na upembuzi wa kimazingira zinaendelea tuna tegemea dampo hilo litaanza kufanya kazi mwezi January.

Mahali ambapo takataka zinamwagwa kwa sasa pamepigwa marufuku kwa sababu hapakidhi vigezo vya kisheria na mazingira.

Katika kutekeleza mkakati wa kufanya mji wa kakonko unakuwa msafi wakati wote ambao uliidhinishwa na baraza la madiwani lilopita idara imepanga ratiba ya kufanya mikutano ya hadhara katika ngazi za vitongoji baada ya kukutana na kamati ya maendeleo ya kata mwishoni mwa mwezi January.

Hata hivyo katika maeneo ya nje ya mji wa kakonko yaani katika kata na vjiji uzoaji wa taka na usafi hufanywa na mpango kata hasa katika masoko na centers hali ya usafi katika masoko yote upo kwa kiwango cha 50%

Katika ngazi ya kaya vijijini wananchi wanadhibiti taka kwa kuchimba mashimo ya taka na wengine kuziweka mashambani kama mbolea.

HIFADHI YA MAZINGIRA

ufuatiliaji wa hifadhi ya mazingira katika kipindi hiki umefanyika katika kufanya ukaguzi wa vyanzo vya maji na maeneo oevu katka kata ya Katanga kasanda Rugenge na Kakonko mjini imeonekana wazi kwamba katika maeneo mengi ardhi oevu na vyanzo vya maji ambavyo kisheria hairuhusiwi kutumika kwa shughuli za kibinadamu wananchi wamelima masebula ndani ya meta 60.hata hivyo kijiji cha Katanga na ilabiro vyanzo vyao vya maji vilivyo vingi wamevihifadhi vizuri.

Miti rafiki wa maji  imepandwa katika vyanzo vya maji vya kata ya Kakonko, Muhange, Kasanda Katanga na maeneo yote kufuatia agizo na uzinduzi wa kuhifadhi mazingira katika vyanzo vya maji uliofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Kakonko tarehe  16 Desemba 2016 ufuatiliaji unaendelea.

Matangazo

  • 94.16% ya WATUMISHI 107 WALIOPANGIWA KURIPOTI TAYARI WAMERIPOTI WILAYANI KAKONKO July 09, 2022
  • WATUMISHI WOTE WOTE WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO NA WAZABUNI WANATANGAZIWA KUFIKA HALMASHAURI KUHAKIKI MADENI YAO YA MWAKA 2021/2022 July 05, 2022
  • TANGAZO LA KUTUMA MAOMBI YA KUJITOLEA KUKIMBIZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA YA KAKONKO MWAKA 2022 July 06, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA MAGARI CHAKAVU KWA NJIA YA MNADA July 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Balozi wa Pamba Tanzania aagiza kampuni iliyonunua pamba kwa mkopo kulipa fedha hizo

    July 31, 2022
  • Wanafunzi wenye mahitaji maalum wang'ara kwenye mashindano

    July 05, 2022
  • WATUMISHI WAPYA 107 WA KADA YA ELIMU NA AFYA WATAKIWA KURIPOTI KWA WAKATI

    July 03, 2022
  • Wazazi wahimizwa kuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ukatili dhidi ya watoto

    June 17, 2022
  • Tazama zote

Video

WATUMISHI KAKONKO WAMPONGEZA MHE.RAIS SAMIA KWA KUONGEZA MISHAHARA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • Pakua hati yako ya malipo ya mshahara Hapa "Utumishi Portal"
  • Halmashauri ya nunua lori na kukabidhi pikipiki 14 kwa Watendaji wa Kata

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa