• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika

 

UTANGULIZI.

Halmashauri kupitia Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa kusimamia shughuli za Idara kama ifuatavyo;  Kutoa ushauri kwa wakulima kuzingatia maelekezo wanayopewa na wataalam wa ugani hususan mbinu mbalimbali za kilimo katika kuvuna na kutunza mazao baada ya kuvuna, Kuungana kukusanya mazao katika vituo vya kukusanyia mazao kupitia vyama vya ushirika (AMCOS) na kuuza kwa pamoja ili kuepuka walanguzi wa mazao na Kutoa tahadhari ya uuzaji holela wa mazao ya chakula unaoweza kupelekea upungufu mkubwa wa chakula ndani ya Wilaya.

Pia tumeendelea kutoa mafunzo na kuhamasisha wakulima juu ya uhifadhi wa mazao katika mifuko bora ya kuzuia mazao kubunguliwa na wadudu, kufanya mikutano na wakulima hasa maeneo ya skimu za umwagiliaji za Katengera na Ruhwiti kuhusu utunzaji wa miundombinu na matumizi mazuri ya maji pamoja na kuandaa mashamba na vitalu mapema ili wazalishe kwa tija. Vilevile tunaendelea kushirikiana na Taasisi na Mashirika mbalimbali kufikisha huduma za ugani kwa wakulima mfano; TARI, FAO, ENABEL, WFP, UNCDF, ITC, TMA na WORLD VISION.

                                                              

HALI YA HEWA.

Kwa kipindi cha robo ya nne hali ya hewa ni mvua kiasi iliyonyesha mwishoni wa mwezi Aprili na Mei mwanzoni ikifuatiwa kiangazi na baridi ya wastani inayoendelea hadi sasa.

 HALI YA CHAKULA

Upatikanaji wa chakula kwa sasa ni mzuri kwani wakulima wanamalizia kuvuna mazao ya msimu huu, hata hivyo kuna dalili za kuwepo kwa upungufu wa chakula kutokana na kasi kubwa ya uuzaji wa mazao ya chakula inayoendelea kutokana na wanunuzi kununua mazao hayo kwa bei ya juu kuliko misimu iliyopita, aidha katika kukabiliana na hali hiyo Halmashauri imewaandikia barua (Kumb. Na. HW/KNK/S.40/VOL.I/58 ya tarehe 20/06/2022) Viongozi wa Serikali za Vijiji na Kata ili kuwashauri wakulima kutouzwa chakula chote kwa lengo la kuondoa hofu ya upungufu wa chakula.

                                                               

HALI YA MAZAO MASHAMBAANI 

4.1 MAZAO YA CHAKULA

Kwa tathmini iliyofanyika kwa robo hii, Hali ya mazao ya chakula kwa sasa inaridhisha hasa baada ya kupata mvua za wastani sehemu kubwa ya Wilaya yetu kwani zaidi ya robo tatu ya malengo ya mavuno imefikiwa licha ya mvua chache iliyonyesha ukilinganisha na misimu mitatu iliyopita.

4.2 MAZAO YA BIASHARA

Wakulima wa zao la tumbaku kwa robo hii wanaendelea na soko la tumbaku, jumla ya mavuno ni tani 165.61(165,609.05Kg) wastani wa hekta limwa ni 115.2 kwa msimu wa kilimo wa 2021/2022. Mazao mengine ni pamba matarajio ya mavuno ni tani 960 (960,000) hekta limwa ni 960, Kahawa tani 24.8 (“Parchment” tani 23.3 na Maganda 1.5, wastani wa hekta limwa ni 48) na Alizeti wastani wa tani 25 zimekamuliwa mafuta na wakulima kuuza mafuta yao wenyewe (Wastani wa hekta zilizolimwa ni 2,022.8 matarajio ni tani 2,528.5).

(Wakulima wanaendelea kukamua alizeti yao kidogo kidogo katika mashine za watu binafsi).   

KAZI ZILIZOFANYIKA

Kitengo Cha Mazao

Kutoa ushauri kwa wakulima kutumia vizuri muda wao katika kilimo hasa kuandaa

    mashamba mapema na kupanda mapema.

Kuwashauri wakulima Kuhifadhi vizuri chakula kilichopatikana na kuuza ziada tu    

Kuanza kwa ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao Kata ya Mugunzu kwa

     kushirikiana na wadau wa kilimo wa Shirika la Enabel.

 Kutoa mafunzo na kuhamasisha wakulima juu ya uhifadhi wa mazao katika mifuko bora ya kuzuia mazao kubunguliwa na wadudu kwa kushirikiana na wadau wa kilimo WFP.  

Kufanya tathmini ya hali ya chakula na upatikanaji wake na kufuatilia hali ya soko la mazao.

Kitengo Cha Ushirika

Katika kipindi hiki Halmashauri imeendelea kutekeleza shughuli za Ushirika kwa kusimamia, kushauri na kuelekeza vyama vya msingi kutekeleza shughuli za ushirika kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za Ushirika nchini kwa kufanya kazi zifuatazo;

  1. Kufanya Mikutano na vyama vya msingi vya ushirika vya Kasuga, Muungano Kiziguzigu, Muhange, Kaziju na Nkuchikeka AMCOS
  2. Kusimamia mikopo ya vyama vya msingi (AMCOS) vya Kizigizigu, Muhange na Kanyonza.
  3. Kusimamia ukusanyaji wa pamoja wa mazao (Maharage) kwa vyama vya msingi vilivyopata mikopo.
  4.  Kuhudhuria kikao cha Mkoani Kigoma kuajadili namna bora ya usimamizi wa ushirika.
  5. Ukusanyaji wa maharage ambapo jumla ya tani 227 zimekusanywa.
  6. Kuwashauri wakulima wa alizeti kuuza kwa pamoja alizeti au mafuta wanayokamua ili kupata bei nzuri na kuirahisishia Halmashauri kukusanya ushuru pamoja na wepesi wa upatikanaji wa takwimu za mavuno.

UPATIKANAJI WA PEMBEJEO.

Katika kipindi cha robo ya tatu hali ya upatikanaji wa pembejeo hasa mbolea siyo mzuri kutokana na mbolea kuuzwa kwa bei kubwa cha kati ya Shilingi 120,000/= hadi 150,000/= kwa mfuko wa kilogram 50. Bei hizo zimewafanya wauzaji wa bidhaa hiyo kushindwa kununua mbolea ya kutosha na kusababisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa mbolea ndani ya Wilaya. Aidha, Mbolea zinazopatikana kwenye maduka ya pembejeo hazitoshelezi mahitaji ya wakulima (mahitaji kwa mwaka ni tani 1887 wakati upatikanaji ni tani 1785). 

CHANGAMOTO

Baadhi kata kutofanya hamasa ya kutosha kwa wananchi juu ya upatikanaji na

     uuzaji wa mbegu za alizeti katika maeneo yao na kupelekea usumbufu kwa wakulima kutopata mbegu kwa wakati na kuifuata Kakonko hali ya kuwa ilipelekwa katika Kata zote.

Uhaba wa watumishi na vitendea kazi kwa maafisa ugani, kwani baadhi ya

      maeneo hakuna maafisa ugani na hivyo wakulima kutopata ushauri unaostahili

      kwa muda muafaka.

Kukosekana kwa Wafanyabiashara wakubwa wa pembejeo za kilimo(Mbolea, Mbegu na Madawa) ndani ya Wilaya.

MIKAKATI 

Kuhamasisha na kuwaelimisha wakulima kulima mazao yanayostahimili ukame kama muhogo na viazi na kutotumia nafaka kwa matumizi yasiyo ya lazima.

Kuendelea kuomba ajira mpya kwa mamlaka zinazohusika na ajira kufikia Ikama itakayotosheleza mahitaji.

Kuwahamasisha Wafanyabiashara ndani ya Wilaya kufanya biashara ya pembejeo za kilimo.


 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa