• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI NA WAZAZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUPINGANA NA UKATILI DHIDI YA WATOTO.

Imetumwa: July 24th, 2025

Wanafunzi wa shule za msingi ambao ni wenyeviti wa kamati za Tuseme shuleni pamoja na walimu wamepatiwa mafunzo kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kumudu mazingira na kupingana na ukatili dhidi ya watoto hususani wasichana wanapokuwa shuleni na katika jamii.

Akifafanua kuhusu mafunzo yaliyotolewa kuanzia tarehe 21-23 Julai, 2025 na kuratibiwa na shirika la UNICEF , Mwalimu William Stephano Kasule kutoka  shule ya msingi kanyonza ambaye ni Mwezeshaji wa mafunzo ya Tuseme na Sara Radio, ameeleza kuwa lengo la mafunzo ni kupinga ukatili dhidi ya Watoto hasa wa kike ambao wamekuwa wakikatiliwa ndoto zao.

Mwezeshaji Mwalimu Kasule ameongeza kuwa washiriki wa mafunzo watatakiwa baada ya kukamilisha mafunzo kwenda kuimarisha kamati za klabu za Tuseme shuleni ambazo zitakuwa zinatumia mbinu mbalimbali kubaini changamoto ili kumlinda mtoto wa kike ambaye amekuwa akifanyiwa ukatili.

Hivyo, wanafunzi hao watakuwa na uwezo mzuri wa kutoa taarifa kwa walimu wao ambao watakuwa ni walezi wa klabu hizi kwa kusaidia kubainisha changamoto zilizopo na kuapata msaada sehemu salama pindi wanapokuwa na ukatili huu. Wengi wao wamekuwa hawajui wapi pa kupata msaada wanapokuwa na taarifa kuhusu ukatili wanaofanyiwa.

“Kupitia hili tunaamini kwamba tunaweza kuleta mapinduzi  makubwa katika kusaidia watoto hawa waweze kupata elimu yao kuanzia shule za msingi, sekondari na elimu ya juu”, alieleza Mwalimu Kasule. 

Sara Joshua Shaluteli, Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kumuhunga ameeleza kuwa wamejifunza namna ya kuwasidia watoto wa kike kujilinda dhidi ya  ukatili unaoendelea katika jamii zao na kutao rai kwa wazazi ambao bado wanashikilia vitendo vya ukatili kuacha kwani vitendo hivyo vinaathiri afya ya akili ya watoto.

Kwa upande mwingine, Aines Daniel, mwenyekiti wa klabu ya tuseme shule ya msingi Gwarama ameahidi kwenda kutoa elimu kwa wanafunzi wengine shuleni kuhusiana na elimu waliyoipata.

“Mimi kama mwenyekiti nitakwenda kuwafundisha wanafunzi shuleni ili na wao wende kuwafundisha wengine kuepuka vitendo vya ukatili dhidi ya watoto  katika jamii”. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO June 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II June 23, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA WASAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II. June 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - WAKUSANYA MAPATO 26 June 21, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • BONANZA LA WATUMISHI KAKONKO DC, KIBONDO DC NA MULEBA DC LAFUNGULIWA RASMI.

    July 26, 2025
  • WANAFUNZI NA WAZAZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUPINGANA NA UKATILI DHIDI YA WATOTO.

    July 24, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUHIFADHI MAZINGIRA NA KUEPUKA MATUMIZI YA VIFUNGASHIO VYA PLASTIKI VINAVYOTUMIKA MARA MOJA.

    June 04, 2025
  • UZINDUZI WA UGAWAJI VYANDARUA KWA WANANCHI WAFANYIKA WILAYANI KAKONKO.

    June 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa