Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kakonko anapenda kuwajulisha kuwa tarehe ya Usaili kwa Wasimamizi wa Vituo, Wasimamizi wasaidizi na Makarani Waongozaji imebadilika kutoka tarehe 08/10/2025 badala yake usaili utafanyika tarehe 10/10/2025 kuanzia saa 3:00 asubuhi.
Aidha, vituo vya kufanyia usaili kanda za usaili hazijabadilika. Msailiwa anatakiwa kufika kwenye usaili akiwa na nyaraka zake zinazomtambulisha ikiwa ni pamoja na mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo;- Kitambulisho cha NIDA, Kitambulisho cha Mpiga kura au Leseni ya udereva.
Mabadiliko haya yamefanyika kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu hivyo tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Kupata majina ya wasailiwa ikiwemo kata ya Kiziguzigu tafadhali fungua hapa chini;
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa