• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Vivutio vya Kitalii

                                             WILAYA YA KAKONKO

TAARIFA YA  VIVUTIO VYA UTALII WILAYA YA  KAKONKO

  • Utangulizi

Wilaya ya Kakonko ni mojawapo ya Wilaya 7 za Mkoa wa Kigoma. Makao makuu ya Wilaya yapo katika Mji wa Kakonko. Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ilianzishwa tarehe 08/3/2013, kwa tangazo la Serikali GN. 287 ya mwaka 2011. Wilaya hii ipo upande wa kaskazini mwa mkoa wa Kigoma kati ya latitudie 3.90 hadi 5.00 kusini na longitudi 30.20 hadi 31.50 mashariki. Wilaya inapakana na Wilaya ya Ngara na Biharamulo (Mkoa wa Kagera) kwa upande wa Kaskazini na Magharibi inapakana na Jamhuri ya Burundi, Kusini inapakana na Wilaya ya Kibondo, Mashariki hadi Kaskazini Mashariki inapakana na Wilaya ya Bukombe (Mkoa wa Geita).

      Ukubwa wa Wilaya

Wilaya ya Kakonko ina ukubwa wa kilometa za mraba 2,219.65 na eneo lililopo ndani ya mamlaka ya Vijiji ni Km za mraba 2,041.03 na eneo la msitu wa hifadhi ni km za mraba 178.62. Wilaya ya Kakonko ina km za mraba 1,084.2 za ardhi inayofaa kwa kilimo na ardhi inayolimwa ni km za mraba 671.8 sawa na 62% ya ardhi inayofaa kwa kilimo. Aidha wilaya ina km za mraba 806.4 ya ardhi ya malisho.

Sehemu ndogo ya Wilaya ya Kakonko ni Hifadhi ya akiba ya wanyamapori ya Moyowosi (Moyowosi Game Reserve) na Msitu wa Hifadhi ya Halmashauri (Buyungu Local Authority Forest Reserve). Maeneo haya ya wanyamapori na Msitu yapo eneo lote la Mashariki kuanzia mpakani mwa Wilaya ya Kibondo hadi mpakani mwa Wilaya ya Bukombe kwa upande wa Kaskazini mashariki. Eneo linalokaliwa na watu limeambaa upande wa magharibi mwa barabara ya Kigoma – Mwanza kupitia Kakonko. Hii inaifanya 38.6% ya Vijiji vyote vya Wilaya ya Kakonko (Vijiji 17) kushirikiana mipaka na nchi ya Burundi kwa urefu wa Km 49.

 

2.0   Hali ya utalii 

Vivutio na Fursa za Utalii zilivyopo katika Wilaya ya Kakonko

Kuona wanyama

Wilaya ya Kakonko inapakana na Pori la akiba la Moyowosi Kigosi lenye hazina kubwa ya wanyama na uoto wa asili. Ukiwa Wilaya ya Kakonko utapata fursa ya kuona hazina kubwa ya Wanyama hawa kama Pundamilia, Tembo, Twiga, Nyati, Simba, viboko, Mamba na Wanyama wadogo kama swala, nyamela, kongoni, kudu, nguruwe pori, nzohe, na samaki aina ya kamongo na kambale. Wanyama hawa ni kivutio kikubwa cha utalii wa ndani na kwa wageni wanaotembelea Wilaya hii. Wilaya inakaribisha wananchi wote na wageni ambao wangependa kutembelea na kuona wanyama na uoto wa asili katika pori hili.

Eneo hili la hifadhi linaweza kufikika kwa urahisi kupitia usafiri wa barabara kutokea Kakonko mjini.

Uwindaji wa Kitalii

Pamoja na kupata fursa ya kuona wanyama, Wilaya ina fursa ya kufanya uwindaji wa kitalii kwa kununua vitalu vya uwindaji katika pori la akiba la Moyowosi Kigosi [Community Based Wildlife Management Areas (CBWMAs)]. Wilaya inakaribisha watalii wa ndani na nje ambao wanatamani kupata fursa hii ya kufanya uwindaji wa Kitalii.

 

Pundamilia katika pori la akiba la Moyowosi Kigosi



 

Maporomoko ya Nyakayenzi

 

Maporomoko haya yanapatikana katika mto mgembezi katika kijiji cha Nyakayenzi kitongoji cha Bizibirinzamba B. Maporoko haya ni kivutio kikubwa cha utalii wa ndani na hata kwa wageni wa naofika katika Wilaya ya Kakonko kwenda kutalii na kuburudika.

 

Mapango ya asili

 

Pango la Nyabubindi [Kasanduka]

 

Pango hili ni la asili na lina ukubwa kiasi cha kuingia watu takribani 50 kwa wakati moja. Pango hili linapatikana katika eneo la mlima Nyamiyaga kitongoji cha Bulembo kijiji cha Nyabibuye Kata ya Nyabibuye. Pango hili ni kivutio cha utalii cha asili kwa Watalii wa ndani na wageni wanaofika katika Wilaya ya Kakonko kwenda kujionea na kufurahi.

 

Pango la Kikulazo

 

Pango hili lipo katika kijiji cha Nyakayenzi kitongoji cha Bizibirinzamba B karibu na maporomoko ya mto Mugembezi. Pango hili linaweza kuingiza watu zaidi ya 15 kwa wakati moja.

 

Pango la Kibika 

 

Kitongoji cha mgembezi kijiji cha Kabare katika milima ya Kibika. Pango hili lina ukubwa wa kuingia watu takribani 20 kwa wakati mmoja. Pango hili lina vitu vya asili vinavyoashiria historia kama michezo ya bao. Pango hili ni kuwa kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na nje.

 

Pango la Ruvumela

 

Pango hili lipo katika kitongoji cha Ruvumela katika kijiji cha Kabare karibu na Mto Mugembezi. Awali pango hili lilitumika kama sehemu ya kufanyia ibada za asili kama matambiko kuomba mvua au hata mabalaa mengine yanayoikumba jamii yaweze kuondoka hivyo ni moja ya kivutio cha utalii.

 

Mahakama ya Mwanzo Kakonko

 

Jengo la Mahakama ya mwanzo Kakonko linasadikiwa kujengwa miaka ya 1920 wakati wa utawala wa kikoloni wa Wajerumani nchini. Jengo hili kwa sasa limekarabatiwa na hivyo kuonekana kama jipya, hata hivyo linabaki kiwa kivutio kikubwa cha utalii kwa watu kwenda na kupata simulizi zake na kujifunza mengi kutokana na historia yake.

 

Nyumba ya Historia ya Ufalme wa WAHA

 

Kama zilivyo tamaduni zingine kuwa na historia ya tawala za kifalme, Kabila la Waha wana historia ya kuwa na utawala wa kifalme [UMWAMI] kabla ya kuja kwa Wakoloni. Historia hii inapatikana katika kijiji cha Itumbiko. Historia hii imehifadhiwa na watalii wanaweza kufika kujionea zana za asili za kabila la Waha kama pinde na mishale, mikuki na tamaduni za mavazi (Mpuzu).

 

Nyumba ya Historia ya Ufalme wa WAHA

 

3.0   Fursa za Uwekezaji  

 

Wilaya ya Kakonko imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi za asili ambazo hazijawekewa uwekezaji wa kutosha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mitaji ya uwekezaji mkubwa na wa ngazi ya kati.

 

3.1 Kilimo

 

Aidha Wilaya ya Kakonko imejaliwa kuwa na hali nzuri ya hewa inayowezesha uwekezaji kuwa mzuri. Ustawi na rutuba nzuri ya udongo uliopo Kakonko hustawisha mazao mbalimbali ya biashara na chakula ikiwemo Pamba, tumbaku, alizeti, mpunga, dengu, mahindi, maharage mtama, mihogo viazi na mihogo.

 

3.2 Mifugo

 

Pia mazingira rafiki pamoja na hali nzuri ya hewa inawezesha ustawi wa mifugo, kama ufugaji wa ngombe, mbuzi, kondoo, kuku, nguruwe na sungura.

 

3.3 Hoteli na Migahawa

 

Halmashauri ya wilaya ya Kakonko imeendelea kujiimarisha kwani kuna nyumba 37 kwa ajili ya kuhifadhi wageni wa kutoka ndani na nje ya Wilaya kwa wakati mmoja. Nyumba hizo ni za viwango cha kati na za kawaida ambazo zinaweza kukidhi mahitaji ya wageni wa aina mbalimbali.  Aidha kuna migahawa ya kutosha na yenye kuvutia inayoweza kutoa huduma ya chakula kizuri kwa wageni mbalimbali.

 

3.4 Stendi ya Kisasa

 

Wilaya ya Kakonko ipo katika hatua za mwisho za kumalizia ujenzi wa stendi ya kisasa katika eneo la Kakonko mjini, barabara ya kuelekea Kibondo. Katika eneo la stendi kuna uwekezaji mzuri wa benki, migahawa, maduka ambayo yatatumika kutoa huduma za usafiri na bidhaa mbalimbali kwa Watalii na jamii kwa ujumla.

 

3.5 Ardhi iliyotengwa kwa uwekezaji

 

Wilaya ya Kakonko imetenga jumla ya Ekari 50 katika maeneo ya Ibuga na Kiziguzizgu kwa ajili ya uwekezaji. Hivyo hakuna usumbufu kwa mwekezaji kupata ardhi hususani kwenye shughuli za utalii.

 

3.5 Maeneo ya makumbusho

 

Wilaya ya Kakonko ina nyumba aliyowahi kuisha Mwalimu Nyerere katika Kata ya Mugunzu. Pia Kuna nyumba aliyokuwa anaishi Chifu (Chifu wa Buyungu) katika Kata ya Kakonko.

 

3.6 Upatikanaji wa Nishati

 

Kwa upande wa nishati, karibu vijiji vyote vina umeme chini ya mpango wa wakala wa umeme vijijini (REA) huku huduma za mitandao ya mawasiliano ya simu zikiwa ni nzuri zinazotolewa na makampuni nya TTCL, Vodacom, Tigo, Aitel, Halotel.

 

4.0 Hitimisho

 

Kwa ujumla fursa za uwekezaji katika Wilaya ya Kakonko ni kubwa hivyo tunawakaribisha wawekezaji wa ndani na nje kuja kuwekeza   katika ili kwa pamoja kuweza kuinua uchumi na kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini hususani katika Nyanja za utalii.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa