• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI ZA VIJIJI ZATAKIWA KUTENGA MAENEO KWA AJILI YA UWEKEZAJI HUSUSANI KILIMO.

Imetumwa: July 31st, 2025

Mkuu wa Wilaya Kakonko kanali Evance Mallasa amewataka Wananchi kupitia Serikali za Vijiji  kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji na kilimo cha kibiashara kwa lengo la kukuza Uchumi wa eneo husika na Uchumi wa mtu mmoja mmoja.

“Serikali za Vijiji zikae na kutenga maeneo ya uwekezaji kisha Serikali italeta miradi na kujenga miundo mbinu”, alieleza Col.Mallasa. 

Katika ziara ya kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi aliyofanya Mkuu wa Wilaya katika kata ya Kasuga na Kanyonza Jumanne 29 Julai, 2025 na kuambatana na Wataalam mbalimbali wa Serikali kuu na Halmashauri, amesisitiza Wananchi kujikita katika ulimaji wa zao la parachichi kisasa pamoja na michikichi.  

Col.Mallasa ameeleza kuwa Wilaya imedhamiria kulima zao la parachichi kibiashara eneo la Mtendeli kata ya Kasanda ambapo zaidi ya hekari 1000 zimetengwa kwa ajili ya kilimo cha parachichi kupitia kilimo cha ‘block farming’ kinachosimamiwa na Wizara ya kilimo ambapo watajenga miundo mbinu, kugawa mbegu, kuleta matrekta, pembejeo na kusimamia kwa karibu ambapo Wananchi watagawiwa maeneo ndani ya kambi ya mtendeli ili kulima parachichi kwa faida na Halmashauri itaweza kupata kipato kupitia ushuru utakaotozwa hapo baadaye.

Mkuu wa Wilaya ameongeza kuwa TARI wataanzisha kituo cha utafiti wa mbegu katika Wilaya ya Kakonko na tayari wameomba eneo kwa ajili ya kuanzisha kituo hicho na taratibu zinaendelea kuwawezesha kupata eneo hilo. Suala hilo litasidia wananchi kupata mbegu bora na utafiti utawezesha wakulima kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika kilimo ikiwemo magonjwa.

Renatus Kagoroba, mkazi wa Kasuga,ameishukuru Serikali kwa kuleta kilimo cha parachichi kwani  ni zao la kudumu hivyo ameomba Serikali kuongeza eneo karibu na eneo lililotengwa kwa ajili ya kilimo cha parachichi ili wananchi walio nje na kata ya Kasanda wapate maeneo kwa ajili ya kulima zao la parachichi pia.

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ameeleza amelichukua hilo na tayari wameanza kulifanyia kazi ili kuwezesha Wananchi walio nje ya kata ya Kasanda kushiriki pia katika kilimo cha parachichi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO June 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II June 23, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA WASAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II. June 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - WAKUSANYA MAPATO 26 June 21, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI ZA VIJIJI ZATAKIWA KUTENGA MAENEO KWA AJILI YA UWEKEZAJI HUSUSANI KILIMO.

    July 31, 2025
  • MDAHALO WA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA WAFANYIKA KAKONKO KWA USHIRIKIANO WA SERIKALI NA UNICEF.

    July 30, 2025
  • BONANZA LA WATUMISHI KAKONKO DC, KIBONDO DC NA MULEBA DC LAFUNGULIWA RASMI.

    July 26, 2025
  • WANAFUNZI NA WAZAZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUPINGANA NA UKATILI DHIDI YA WATOTO.

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa