• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Utumishi na Utawala

1.0 UTANGULIZI

Wilaya ya Kakonko ina jumla ya Tarafa tatu (3) ambazo ni Nyaronga, Kasanda na Kakonko ambazo zina jumla ya Kata kumi na tatu (13), vijiji 44 na Vitongoji 355.

Utawala bora na uwajibikaji ni mojawapo ya maeneo muhimu yanayopewa kipaumbele na Serikali kupitia Ilani ya uchaugzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, Dira ya maendeleo ya Taifa 2025, Mkakati wa Maendeleo Endelevu (SDG) na Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano (2021/2022 – 2025/2026).

Kero na malalamiko mbalimbali ya wananchi hutatuliwa kupitia Ofisi za Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji, Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wa Kata, Mkurugenzi Mtendaji, Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Aidha Halmashauri ina dawati maalumu linaloshughulikia malalamiko mbalimbali yanayoletwa dhidi ya Halmashauri au Watendaji wake na kufanya ufuatiliaji kuhakikisha kila lalamiko la mwananchi linatatuliwa au kuelekezwa kwenye mamlaka inayohusika. Baadhi ya malalamiko ama kero ni kama Migogoro ya Ardhi, Migogoro ya unyanyasaji wa Kijinsia na mingine. Kero nyingi hutatuliwa kupitia dawati la malalamiko kwa kuwasiliana ama kushirikiana na wahusika wa maeneo au idara husika. Pia masanduku ya maoni yamewekwa katika Ofisi ili kubaini kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi mapema.

2.1 Hali ya Watumishi katika Halmashauri 

Hali ya watumishi katika miaka miwili iliyopita hadi sasa ni kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini. Kwa sasa Halmashauri inauhitaji wa watumishi 1958 sawa na 50% kama ifuatavyo;


Mwaka

Mahitaji

Waliopo

Upungufu

Upungufu %

2020/2021

1958

951

1,007

49%

2021/2022

1958

988

970

50%


Chanzo: Idara ya Utawala na Utumishi

2.2 Watumishi wapya walioajiriwa katika kipindi cha miaka miwili .

Katika Kipindi cha miaka 2 Halmashauri imefanikiwa kupata ajira mpya kwa Kada tofauti tofauti kama mchanganuo ufuatao unavyoonesha:

Mwaka

Idadi ya Watumishi walioajiriwa

Idara ya Utawala

Idara ya Afya

Idara ya Elimu Msingi

Idara ya Elimu Sekondari

Idara ya Ujenzi

2020/2021

34

1

0

17

16

0

2021/2022

49

0

23

17

8

1

Halmashauri imekuwa ikitenga katika bajeti kwa ajili ya ajira mpya kwa kila mwaka wa fedha ili kuhakikisha Halmashauri iweze kupata watumishi wa kutosha ili kuweza kutoa huduma nzuri kwa wananchi.

 

2.3 Ujenzi wa nyumba za Watumishi

Halmashauri imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi Mtendaji na inaendelea na ujenzi wa nyumba 2 za Wakuu wa Idara ambapo hadi kufikia  mwezi Septemba  2022 ujenzi wa nyumba mbili za wakuu wa idara umefikia hatua ya umaliziaji kwa ujenzi wa  nyumba ya kwanza (moja) na hatua ya msingi kwa nyumba ya pili.

2.4 Ujenzi wa Majengo ya Utawala

 

Katika kipindi cha 2019/2020 hadi 2021/2022 Halmashauri imeendelea na ujenzi wa jengo la utawala awamu ya III ambapo hadi kufikia Sept 2022 ujenzi upo hatua za mwisho za umaliziaji.

2.5 Mkakati wa kuwabakiza watumishi

Halmashauri ameandaa mkakati wa kuwabakiza watumishi ili kupunguza idadi ya watumishi wanaohama kwa kufanya yafuatayo:

 

2.5.1 Kutoa motisha kwa watumishi wapya na waliopo.

Kuwepo kwa malazi, chakula na viburudisho wakati wa mapokezi.

Kuwepo kwa mapokezi na usafiri kutoka stendi kuu ya wilaya ya Kakonko.

Uwepo wa nyaraka mbalimbali zinazohusiana na ajira.

Watumishi wapya Kupewa vifaa vya kuanzia kazi kama vile magodoro na mitungi midogo ya gesi.

Matumizi ya lugha nzuri kwa watumishi wapya wakati wa mapokezi.

Fedha za kujikimu kwa watumishi wapya itolewe kwa wakati.

Masuala yahusuyo mishahara yashughulikiwe kwa wakati.

Kutengeneza mazingira rafiki ya upatikanaji wa viwanja vya makazi kwa kuwapunguzia kuanzia aslimia 20-30; iliwahamasike kujenga nyumba zao na hatimaye wayafanye makazi yao ya Kakonko kuwa ya kudumu.

Kuwepo kwa usafiri wa kuwapeleka watumishi wapya kwenye vituo vyao vya kazi.

Mwajiri kutoa lori kwa watumishi wanaojenga ili wao wagharimie mafuta wakati wa kusomba vifaa vyao vya ujenzi.

  • Mwajiri kujenga hosteli/Nyumba ya kulala wageni ya biashara kwaajili ya kuiingizia Halmashauri mapato ambapo pia itatumika kuwapokelea watumishi wapya.

Watumishi waliopo.

  • Kujengwa kwa kituo cha kujisomea (Resource centre).

Kutolewa kwa mikopo nafuu.

Kutengeneza mazingira rafiki kati ya watumishi na jamii inayowazunguka kwa kuwepo kwa kikosi kazi maalum kitakachozunguka wilaya nzima.

Kuboresha utoaji wa huduma/utoaji wa huduma kwa wakati.

Kuwepo kwa mabonanza mbalimbali ya michezo ili kuondoa ombwe lililopo kati ya watumishi wa makao makuu na wale waliopo kwenye vituo vya kutolea huduma.

Kuboresha miundo mbinu katika vituo vya kutolea huduma mfano nyumba za kuishi.

Kutengeneza mazingira rafiki ya upatikanaji wa viwanja vya makazi.

Kuwatambua watumishi wanaofanya vizuri katika kazi zao na kuwapa motisha mbalimbali kama vile kupelekwa sehemu za utalii na kupewa madaraka.

Mkurugenzi aandae usafiri wa kwenda na kurudi makao makuu ya Halmashauri kwaajili ya watumishi wa makao makuu.

Mwajiri alipe kwa wakati stahiki za uhamisho kwa watumishi wanaohama vituo ndani ya Halmashauri na wale wanaohamia kutoka nje ya Halmashauri.

Mwajiri kuwapunguzia watumishi bei za viwanja ili wahamasike kujenga nyumba zao na hatimaye wayafanye makazi yao ya Kakonko kuwa ya kudumu.

Mwajiri kutoa lori kwa watumishi wanaojenga ili wao wagharimie mafuta wakati wakusomba vifaa vyao vya ujenzi.

Mwajiri kujenga hosteli/Nyumba ya kulala wageni ya biashara kwaajili ya kuiingizia Halmashauri mapato ambapo pia itatumika kuwapokelea watumishi wapya.

Halmashauri kutengeneza maeneo mbalimbali ya starehe yatakayowafanya watumishi na familia zao kuwanasehemu za kupumuzika na kufurahi kama ilivyo miji mingine.

  • Kutoa mafunzo kwa watumishi wanaotarajiwa kustaafu kazi kwa kuwapatia mbinu mbalimbali za namna ya kuishi baada ya kustaafu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa