• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI KAKONKO ROBO YA TATU 2024/2025 LAWEKA MKAZO MAENDELEO, UWAJIBIKAJI NA USHIRIKIANO WA PAMOJA.

Imetumwa: May 21st, 2025


Kakonko, 20 Mei 2025 – Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko limefanya kikao chake cha robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2024/2025, kikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Fidel Chiza Nderego, aliyeeleza kuwa hali ya halmashauri ni nzuri na ushirikiano miongoni mwa viongozi umeimarika, hivyo akatoa wito wa kuendeleza mshikamano huo kwa maslahi ya wananchi.

Katika mkutano huo, wenyeviti wa kamati mbalimbali waliwasilisha taarifa na hoja mbalimbali zikiangazia utekelezaji wa shughuli za maendeleo, ustawi wa jamii na utawala bora.

Kamati ya kudhibiti UKIMWI ilijadili upatikanaji wa mipira ya kike ya kujikinga, ambapo Mwenyekiti aliahidi kuwa vifaa hivyo, vilivyoagizwa pamoja na vifaa vingine vya hospitali, vitapatikana ndani ya wiki moja.

Kamati ya Maadili ilitoa pongezi kwa madiwani wote kwa kutokuwa na malalamiko ya ukiukwaji wa maadili katika kipindi cha robo hii, hali inayoonesha nidhamu na uwajibikaji miongoni mwao.

Kamati ya Elimu, Afya na Maji ilitoa hoja ya kuongeza shule ya sekondari katika Kata ya Gwarama ili kupunguza umbali wa wanafunzi. Mkurugenzi Mtendaji, Ndaki Stephano Mhuli, alieleza kuwa serikali inaendelea na ujenzi wa shule kila mwaka, na kwamba Gwarama iko kwenye mpango huo. Aliongeza kuwa shule ya Sekondari Muhange inapendekezwa kuwa shule ya upili (high school), na ujenzi wa shule mpya katika kijiji cha Mbizi pia upo kwenye mipango.

Kamati ya Huduma za Kiuchumi, Ujenzi na Mazingira iliwasilisha taarifa yake bila hoja yoyote kuibuliwa, huku kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ikijadili changamoto ya upatikanaji wa fedha za walengwa wa TASAF. Mkurugenzi Mtendaji alifafanua kuwa changamoto hiyo ilitokana na mabadiliko ya kimfumo katika ngazi ya kitaifa baina ya mifumo ya benki na serikali, lakini fedha hizo zitarudishwa kwa walengwa.

Afisa kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Uongozi, Patrick Shayo, aliwakumbusha viongozi wote wa umma kuwasilisha tamko la rasilimali na madeni kila mwaka kabla ya tarehe 30 Desemba kupitia mfumo wa ODS, huku viongozi wanaomaliza muda wao wakitakiwa kuwasilisha tamko hilo ndani ya siku 90.

Meneja wa NHIF Mkoa wa Kigoma, CPA Gwamaka Alfred Mtalila, alieleza kuhusu utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote na kuhimiza wananchi kujiunga na bima kupitia kitita cha jamii kwa Tsh 150,000 kwa mwaka. Alibainisha kuwa huduma hiyo inajumuisha huduma 277, huku TASAF ikitumika kuwaainisha wananchi wasio na uwezo ili kupata bima hiyo kwa msaada wa serikali.

Mwakilishi wa Meneja wa SIDO Kigoma, Mhandisi Alexander Nicholaus Mpuya, alieleza majukumu ya shirika hilo katika kusaidia viwanda vidogo, masoko, mikopo na ushauri wa kibiashara. Alieleza kuwa SIDO imesaidia ujenzi wa viwanda vidogo katika kata ya Gwarama, Kiga na Muhange. Alitoa wito kwa wananchi kushiriki mafunzo ya uendeshaji wa biashara.

Mkurugenzi Mtendaji, Ndaki Stephano Mhuli, alieleza mafanikio ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo:

Ujenzi wa vibanda vya soko la Kakonko unaokamilika mwezi Mei 2025, na utazinduliwa rasmi tarehe 1 Juni 2025.

Ujenzi wa stendi mpya ya mabasi unaotarajiwa kukamilika na kukabidhiwa ifikapo tarehe 30 Juni 2025.

Kupokea watumishi wapya 40 katika kada mbalimbali.

Ziara ya mafunzo Wilayani Muleba kuhusu kilimo cha ‘block farming’ ambapo ekari 1,530 zimetengwa kwa ajili ya mazao kama parachichi, kwa vijana, wanawake na makundi mengine.

Kuhusu zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililofanyika kuanzia tarehe 1 hadi 7 Mei 2025, zaidi ya wananchi 4,851 waliandikishwa na jina la jimbo likabadilishwa kutoka Buyungu na sasa kuitwa Jimbo la Kakonko.

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya, pamoja na mwakilishi wa mkoa Bw. Moshi Hussein Muhini, waliipongeza Wilaya kwa usimamizi mzuri wa miradi na kuhimiza kukamilisha miradi yote ifikapo tarehe 15 Juni 2025, pamoja na kufanyia kazi hoja za CAG.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kakonko, Ndugu Saamoja Sadock Ndilaliha, alisifu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na ushirikiano wa kisiasa, akisisitiza kuwa siasa siyo uadui bali ni jukwaa la kushirikiana kwa maendeleo ya wananchi.

Katibu wa Baraza alitoa shukrani kwa viongozi wa idara, dini, siasa na madiwani kwa ushirikiano mzuri ambao umechangia ongezeko la mapato ya halmashauri kutoka chini ya bilioni moja hadi kufikia bilioni 1.88.

Akifunga kikao, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Fidel Chiza Nderego, aliwashukuru madiwani kwa uvumilivu na mchango wao katika maendeleo, na kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji kwa usimamizi mzuri wa miradi, huku akiahidi kuwa halmashauri itaendelea kuwa mfano wa kuigwa katika maendeleo ya wananchi wa Kakonko.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II June 23, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA WASAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II. June 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - WAKUSANYA MAPATO 26 June 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI. June 21, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAASWA KUHIFADHI MAZINGIRA NA KUEPUKA MATUMIZI YA VIFUNGASHIO VYA PLASTIKI VINAVYOTUMIKA MARA MOJA.

    June 04, 2025
  • UZINDUZI WA UGAWAJI VYANDARUA KWA WANANCHI WAFANYIKA WILAYANI KAKONKO.

    June 03, 2025
  • PSSSF YARAISISHA HUDUMA KWA WASTAAFU KUPITIA MIFUMO YA KIDIJITALI.

    May 29, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KAKONKO ROBO YA TATU 2024/2025 LAWEKA MKAZO MAENDELEO, UWAJIBIKAJI NA USHIRIKIANO WA PAMOJA.

    May 21, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa