• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

PSSSF YARAISISHA HUDUMA KWA WASTAAFU KUPITIA MIFUMO YA KIDIJITALI.

Imetumwa: May 29th, 2025

Na Cosmas Makalla - Kakonko

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeanzisha mifumo miwili ya kidijitali inayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wanachama wake, hususan wastaafu, kwa kurahisisha mchakato wa kuomba na kupata mafao.

Mifumo hiyo miwili PSSSF Portal na PSSSF Kiganjani inamwezesha mwanachama kuwasilisha maombi ya mafao, kuangalia michango yake, kuongeza wategemezi, na kupata huduma nyingine kwa njia ya mtandao au kupitia simu ya mkononi.

Akizungumza katika kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kilichofanyika makao makuu ya halmashauri hiyo leo Alhamisi 29 Mei, 2025, Meneja wa PSSSF Mkoa wa Kigoma, Bwana Sayumwe Yotham, alisema kuwa lengo la mifumo hiyo ni kurahisisha huduma na kupunguza adha ya wateja kusafiri hadi ofisi za mfuko.

“Kwa sasa mwanachama anaweza kuangalia taarifa zake binafsi za michango na kuwasilisha maombi ya mafao akiwa mahali popote, muda wowote,” alisema Bw. Sayumwe.

Kwa mujibu wa Bw. Sayumwe, PSSSF Portal inapatikana kupitia tovuti kwa kuingia katika injini ya utafutaji ya Google na kutafuta “PSSSF Portal”, ambapo mwanachama atatakiwa kujisajili ili kuanza kutumia huduma.

Kwa upande mwingine, PSSSF Kiganjani ni programu ya simu inayoweza kupakuliwa kupitia Play Store. Baada ya kupakua, mwanachama anaweza kuanza kutumia mfumo huo kwa shughuli mbalimbali za huduma.

Meneja huyo alitaja baadhi ya faida za mifumo hiyo kuwa ni pamoja na:

  • Uwezo wa kuwasiliana moja kwa moja na mfuko bila kwenda ofisini,
  • Uwazi wa taarifa kati ya mwanachama na PSSSF,
  • Urahisi wa kupata huduma katika maeneo ya mbali,
  • Kupunguza ucheleweshaji wa mafao kwa wastaafu.

PSSSF inatoa mafao mbalimbali ambayo sasa yote yanaweza kuombwa kwa njia ya mifumo hiyo. Mafao hayo ni pamoja na:

  • Fao la Kustaafu, linalolipwa kwa awamu mbili kwa wale wanaostaafu kwa hiari (miaka 55–59) au kwa lazima (miaka 60),
  • Fao la Urithi, linalotolewa kwa wategemezi wa mwanachama aliyefariki,
  • Fao la Ulemavu wa Muda Mrefu, linalotolewa kwa walioathirika nje ya mazingira ya kazi,
  • Fao la Kifo, kwa mjane/mgane na watoto wa mwanachama aliyefariki,
  • Fao la Uzazi, kwa mwanamke aliyekuwa mwanachama aliyechangia kwa miezi 36,
  • Fao la Kukosa Ajira, kwa waliofukuzwa kazi (siyo waliokoma kwa hiari).

Kuanzia tarehe 1 Januari 2025, PSSSF imeongeza mafao mawili mapya:

  1. Fao la Msaada wa Mazishi, linalotolewa iwapo mwanachama atafariki na taarifa ya kifo itatolewa ndani ya siku 30.
  2. Fao la Mkupuo wa Miezi 36, ambapo wategemezi wa mwanachama aliyefariki hulipwa mkupuo wa miezi 36 ya michango.

Aidha, Bwana Sayumwe amewahimiza watumishi wa umma kuhakikisha wanaomba mafao yao miezi sita kabla ya kustaafu, mara tu baada ya kupata kibali cha kustaafu, ili kuhakikisha wanalipwa kwa wakati bila ucheleweshaji.

“Ni muhimu wastaafu wanaotarajiwa wakaanza mchakato mapema kwa kutumia mifumo hii ili kuhakikisha mafao yao yanapatikana mara moja baada ya kuhitimisha utumishi wao,” alisisitiza, Meneja Sayumwe.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PSSSF YARAISISHA HUDUMA KWA WASTAAFU KUPITIA MIFUMO YA KIDIJITALI.

    May 29, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KAKONKO ROBO YA TATU 2024/2025 LAWEKA MKAZO MAENDELEO, UWAJIBIKAJI NA USHIRIKIANO WA PAMOJA.

    May 21, 2025
  • HALMASHAURI KUU YA WILAYA YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) YA KAKONKO YAPONGEZA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJI KAZI MZURI WA KAZI KWA VIONGOZI.

    May 14, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KAKONKO

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa