• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Balozi wa Pamba Tanzania aagiza kampuni iliyonunua pamba kwa mkopo kulipa fedha hizo

Imetumwa: July 31st, 2022

Balozi wa Pamba Tanzania Aggrey Mwanri amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa kufuatilia kampuni iliyonunua kwa mkopo tani 9 za pamba katika Chama cha Ushirika Kanyonza (AMCOS) ili fedha hizo zilipwe mara moja. 

Akipokea taarifa ya majumuisho ya kampeni ya pamba kuongeza tija na uzalishaji katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri  Jumapili tarehe 31.07.2022, Balozi wa pamba ameagiza makampuni yatafutwe na kulipa fedha hizo mara moja.

“Tunadai kampuni ya Mbogwe and Bukombe Cooperative Union Ltd (MBCU)  wastani wa tani 9 yenye thamani ya milioni 17, fedha hiyo ikipatikana wakulima watakuwa na Imani na sisi”, alieleza bwana Feniasi Raphael Damas, Mwenyekiti wa AMCOS Kanyonza.

 Bwana Renatus Luneja afisa kilimo wa bodi ya pamba na mwakilishi wa  Mkurugenzi wa bodi ya pamba alieleza kuwa kwa mujibu wa taratibu hairuhisiwi kununua  pamba kwa mkopo kwani kampuni inatakiwa kufika na fedha taslimu na kuwalipa wakulima kituoni hivyo ni uzembe wa viongozi wa Chama cha Ushirika. Alimwomba mkuu wa Wilaya kushirikisha bodi ya pamba wakati anachukua hatua na wao watashirikiana naye kwa nguvu zote.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kakonko ndugu Saamoja Ndilaliha alisisitiza wakulima wa pamba walipwe fedha zao ndani ya siku saba.   Alieleza hana mashaka na utendaji kazi mzuri wa Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa alieleza tayari aliwaita viongozi wa AMCOS Kanyonza baada ya kupata taarifa kuwa pamba imechukuliwa kwa mkopo na kufanya kikao nao hivyo ufuatiliaji wa karibu unaendelea ili fedha za pamba iliyochukuliwa ilipwe. Hata hivyo alihimiza viongozi wa AMCOS kuwaacha wakulima wachague kampuni ya kuuzia pamba yao kwani hapakuwa na haja ya kuuza pamba kwa kampuni ambayo ilikuwa haina fedha na kuacha kampuni iliyokuwa na fedha hivyo aliahidi kuchukua hatua.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli aliahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na balozi wa pamba Tanzania na viongozi wengine.

Matangazo

  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA ZA MRADI WA BOOST TSHS.1,457,800,000 May 03, 2023
  • 94.16% ya WATUMISHI 107 WALIOPANGIWA KURIPOTI TAYARI WAMERIPOTI WILAYANI KAKONKO July 09, 2022
  • WATUMISHI WOTE WOTE WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO NA WAZABUNI WANATANGAZIWA KUFIKA HALMASHAURI KUHAKIKI MADENI YAO YA MWAKA 2021/2022 July 05, 2022
  • TANGAZO LA KUTUMA MAOMBI YA KUJITOLEA KUKIMBIZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA YA KAKONKO MWAKA 2022 July 06, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KWA KUSHIRIKIANA NA REDESO WATOA ELIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA KWA WAKAZI WA KATA YA KASANDA.

    May 23, 2023
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WILAYANI KAKONKO YAHIMIZWA KUTOA HUDUMA KWA KUZINGATIA MISINGI YA MAADILI YA KITANZANIA.

    May 17, 2023
  • WATAALAM WA AFYA WASISITIZA WANANCHI KUZINGATIA MATUMIZI YA VYOO BORA.

    May 12, 2023
  • MFUKO WA JIMBO LA BUYUNGU WAKABIDHI SARUJI 100 ZA UKARABATI WA MADARASA 5 SHULE YA SEKONDARI KASHOZA.

    May 09, 2023
  • Tazama zote

Video

Kaya 263 za TASAF kata ya Kasanda Wilayani Kakonko zampongeza Rais Samia kwa kuboresha maisha yao.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa