• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Baraza la Madiwani lakataa miradi 4 ya maji na kumwondolea majukumu Mkuu wa Idara

Imetumwa: March 1st, 2018

Baraza la madiwani Wilayani Kakonko limekataa kupokea miradi ya maji wa Vijiji 4 uliokuwa ukitekelezwa tangu mwaka 2012 na kumuondolea majukumu mkuu wa Idara ya maji kupisha uchunguzi katika kikao cha robo ya pili kilichofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Akitoa maamuzi ya Baraza la madiwani, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye alikuwa akiendesha mkutano huo, Toyi Butono alieleza kuwa wamechukua hatua hiyo baada ya kuona miradi ya maji ya Vijiji 4 imekamilika lakini ina kasoro nyingi hivyo wananchi kushindwa kupata huduma ya maji.

“Madiwani wa Chama cha Mapinduzi pamoja na madiwani wa upinzani kwa pamoja tumekataa miradi ya maji ya Vijiji vinne vya Nyagwijima, Kiduduye, Katanga/Ilabiro na Muhange na tunamuondolea majukumu ya ukuu wa Idara Mhandisi wa Maji ili kupisha uchunguzi.” alisema makamu Mwenyekiti.

Mhandisi wa maji aliyeondolewa majukumu yake ya ukuu wa Idara ili kupisha uchunguzi ni injinia Elinathan Eliya Mkuu wa Idara ya maji aliyekuwa akisimamia miradi hiyo kwa kushirikiana na Wilaya ya Kibondo.

Skimu ya maji ya vijiji vya Muhange, Nyagwijima, Kiduduye, Katanga/Ilabiro na Kiga ni miradi iliyoingizwa katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na kutekelezwa pamoja na miradi mingine ya Kibondo.

Ujenzi wa skimu ya maji kijiji cha Muhange ulianza Desemba 2012 na Mkandarasi aliyejenga mradi huu ni Famoyo Contractors kutoka Kasulu. Halmashauri ya Wilaya Kibondo ndiyo iliyosaini Mkataba wa Mradi huu na ndiye aliyekuwa msimamizi mkuu wa Mradi akishirikiana na mhandisi wa Halmashauri ya Kakonko. Gharama za Mradi ni Tsh 820,591,309.90.

Aidha mradi wa Skimu ya maji ya kijiji cha Kiduduye  ulianza mwaka 2013 na mkandarasi Karago Enterprises toka Dodoma.

Kwa upande wa mradi wa Skimu ya maji vijiji vya Katanga na Ilabiro ulianza mwaka 2013 na mkandarasi aliyesaini mkataba huu ni kampuni ya Y.N investment kutoka Dar es salam. Halmashauri ya Wilaya Kibondo ndiyo iliyoratibu shughuli za ushauri wa kitalaaam baada ya Mtalaam mshauri kusitishwa mkataba wake.

Mradi wa Skimu ya maji kijiji cha Nyagwijima ulianza desemba 2012 na Mkandarasi aliyejenga mradi huu ni Karago Enterprises kutoka Dodoma.

Miradi hiyo ilikuwa ikitekelezwa katika Vijiji 5 ambapo mradi wa maji wa Kijiji cha Kiga ndio pekee uliokubaliwa na Baraza la Madiwani kutokana kufanya kazi vizuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa