Mkutano maalum wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya Wilaya ya Kakonko imempongeza Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa, kwa uwajibikaji na utendaji kazi mzuri wa kazi katika kuitekeleza ilani ya CCM kwa kipindi cha julai hadi desemba 2024 ambapo wamemuomba kuchukua pongezi pamoja na ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na wajumbe lengo ikiwa ni kuendelea kuboresha utekelezaji wa ilani ya chama inayounda serikali.
Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 14 mei 2025, na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kakonko Ndg.Saamoja S.Ndilaliha,wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo wilayani kakonko,kupitia mkutano huo pia wamempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndg.Ndaki Stephano Mhuli,pamoja na menejimenti kwa ujumla kwa kazi nzuri wanazozifanya ikiwa ni utekelezaji wa ilani jambo ambalo linapelekea wananchi kuendelea kuimini Serikali kupitia Sekta ya mbalimbali ambazo zinagusa wananchi wote.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani Col.Mallasa, ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuboresha na kusogeza huduma zote kwa wananchi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo mradi wa maji. ameeleza RUWASA wilaya ya kakonko inatarajia kuongeza huduma ya upatikanaji wa maji kutoka asilimia 88.3 ya sasa hadi kufikia aslimia 91.2 sawa na ongezeko la asilimia 2.9 za upatikanaji wa huduma ya maji vijijini ameeleza ongezeko hilo litakuwa limevuka lengo la ilani ya chama cha mapinduzi kwa asilimia 6.2,ameeleza wilaya ya kakonko imeendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025,ilani ambayo inaendelea na mapambano dhidi ya umasikini,ukosefu wa ajira,rushwa, kudumisha umoja,amani pamoja na ulinzi na usalama.
Kwa upande wa nishati ameeleza kuwa TANESCO na REA wanaendelea kusambaza nishati ili kuwafikia wananchi wote. aidha elimu ya matumizi bora ya nishati inaendelea kutolewa kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya nishati inapopita lengo ikiwa nikuwajengea uwezo watumiaji wa nishati ya umeme.
Mbali na hayo, ameeleza kama wilaya wamejipanga kikamilifu kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama inaendelea kuwa vizuri huku akiwataka kuendelea kushirikiana,kushauriana na kusaidiana kwa pamoja katika maeneo yao kuhakikisha hali ya usalama inaimalika zaidi.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa