• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

Imetumwa: March 3rd, 2025

Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Mhe.Aloyce Kamamba, leo Jumatatu Machi 03, 2025 amekutana na kufanya kikao na Watumishi wa Halmashauri wa makao makuu huku akiwasisitiza kutumia rasiliamali na fedha zinatolewa na Serikali vizuri,  kujiendeleza kielimu, kuwekeza na kujiandaa kustaafu.

Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri wanaofanya kazi katika ofisi za Halmashauri eneo la Kanyamfisi, Mhe.Kamamba amewasisitiza Watumishi kila mmoja kwa eneo lake kusimamia vizuri rasilimali na fedha zinazotolewa na Serikali ili kuleta manufaa katika jamii na vizazi vijavyo.

“Tuwe waaminifu kwenye kazi tunazopewa ili zitusaidie kupanda hatua inayofuata katika kazi zetu”, alieleza Mbunge wa Jimbo la Buyungu.

Aidha Mbunge ameongeza kuwa pamoja na kazi wanazofanya za kutumikia Wananchi, Watumishi  wanapaswa kuanza kuwekeza kwa kujikita katika shughuli za maendeleo ikiwemo kilimo na biashara kwa ajili ya maisha ya baadaye na kujiandaa kustaafu.

Mhe.Mbunge amefafanua kuwa kutunza fedha siyo jambo rahisi badala yake ni vizuri kuwekeza fedha kwa kujikita katika shughuli za ujasiriamali na miradi mara baada ya masaa ya kazi.

Vilevile, Mhe.Kamamba amewahimiza Watumishi wajiendeleze kieleimu na kitaaluma kwani elimu inaongeza thamani ya mtu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Michael Faraay amempongeza Mhe.Mbunge wa Jimbo la Buyungu kwa nasaa nzuri alizotoa kwa Watumishi na kuahidi kufanyia kazi yale aliyoyaeleza kwa manufaa ya Watumishi na jamii kwa ujumla.

Mhe.Fidel Chiza Nderego, Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye ameshiriki kikao hicho ameeleza watatoa ushirikiano wa dhati kwa jitihada anazofanya mheshimiwa mbunge kuleta maendeleo kwa Jimbo la Buyungu na Wananchi kwa ujumla.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Watumishi wameleza kufurahishwa na hatua ya Mheshimiwa Mbunge kuandaa kikao na kuzungumza na Watumishi huku akiwaasa kujikita katika uwekezaji na kujiandaa kustaafu kwani mambo hayo yataleta tija kwa Watumishi wote watakapozingatia na kuyatekeleza.

Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Buyungu, anafanya ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Jimbo akifanya mikutano na Wananchi, kugawa mashine za kudurufu kwenye ofisi za kata 13 ambapo zitatumika pia katika shule za msingi na sekondari zilizopo ndani ya kata.

Ziara hiyo imeanza tarehe 28.02.2025 na itamalizika tarehe 09.03.2025 ikihusisha Wataalam mbalimbali wa Halmashauri ambao wanatoa ufafanuzi kwa Wananchi kuhusiana na masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa