Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kigoma ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Thobius Andengenye Leo Julai 30,2023 imefanya ziara ya kutembelea miradi inayotarajiwa kutembelewa, kuwekewa jiwe la Msingi na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru Agosti 16,2023.
Kamati hiyo imetembelea miradi (08) ikiwemo Ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Wilaya (Ikulu ndogo), Ujenzi wa Ofisi ya Afisa Tarafa Kasanda, Barabara ya Lami Kakonko – Itimbiko, Shule ya Wasichana Kakonko, Mradi wa kuzalisha mkaa mbadala-Itumbiko, Kituo Cha Mafuta Glory to God, Zahanati ya Ilabiro, pamoja na Kikundi cha Vijana Azimio Kiziguzigu.
Aidha CGf (Rtd) Andengenye amewataka wasimamizi wa Miradi hiyo kuhakikisha wanafanyia kazi mapungufu yaliyosalia katika miradi hiyo Ili kuepuka kukataliwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kakonko Kanali Evance Mesha Mallasa, amewasisitiza wasimamizi wa miradi kuzingatia na kutekeleza Maelekezo yaliyotolewa ili kuepuka kurudia maelekezo yaleyale kila wakati.
Vile vile Kanali Mallasa amesisitiza Kuendelea kufanya kazi kwa kushirikiana baina ya wasimamizi wa miradi na idara husika ili miradi ikamilike kwa ufanisi.
"Natamani nikimwambia Mtu kitu kama atashindwa kufanya aje aniambie, tukisema Barabara isafishwe isafishwe, tusiwe Watu wa kukaa kimya tukishirikiana tukazumgumza hakuna kinacho shindikana"amesema Kanali Mallasa.
Mwenge wa uhuru unatarajiwa kupokelewa Kimkoa Wilayani Kakonko Agosti 16,2023, ukitokea Mkoa wa Kagera.
Kauli mbiu ya Mwaka huu "Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya maji kwa ustawi wa viumbe hai na uchumi wa Taifa".
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa