• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya Kakonko atoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Tshs.100,800,000 kuwezesha nyumba 46,857 kupata anuani za makazi.

Imetumwa: March 19th, 2022


Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Evance Mallasa ametoa  shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Tshs.100,800,000 (milioni mia moja na laki nane) ambazo zitawezesha nyumba 46,857 kupata anuani za makazi.

Akizindua  rasmi zoezi la anuani za makazi kwa kuweka namba katika nyumba mbili za Wananchi na kibao cha barabara ya Anglikana na Mkakila siku ya Ijumaa tarehe 18.03.2022.

Mkuu wa Wilaya ambaye alikuwa mgeni rasmi amewasisitiza vijana 200 watakaofanya kazi hiyo kutumia maelekezo na mafundisho waliyopata kuwaelekeza Wananchi umuhimu wa zoezi hili.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndaki S.Mhuli ameeleza kuwa Serikali imetoa Tshs.100,800,000 (milioni mia moja na laki nane) kwa ajili ya zoezi la anuani za makazi ambapo makundi yote yamewezeshwa ikiwemo watendaji wa Vijiji ambao wamepewa elimu kisha kukaa na kupendekeza majina ya Vijiji na mitaa kisha kushiriki zoezi la kuweka namba kwa nyumba ambalo tayari limefanyika.

Mkurugenzi ameeleza kwa sasa zoezi litakalofanyika ni kuchukua taarifa za kila nyumba.

“Tunaomba wananchi watusaidie kutoa ushirikiano wa kubandika vibao kwenye nyumba zao na kugharamia wenyewe vibao hivyo”, Alieleza Mkurugenzi Mtendaji.

Mratibu wa zoezi la anuani za Makazi Gideon Kimaro ametoa taarifa kuwa zoezi hilo linafanyika kwa kuzingatia sera ya Posta yam waka 2003 na Ilani ya Chama cha Mapinduzi yam waka 2020- 2025.

“Wilaya ya Kakonko ina  Tarafa 03, Kata 13, Vijiji 44 na Vitongoji 355 ambapo nyumba 48,857 zimesajiliwa na kuandikwa namba kwenye kuta zake”, ameeleza mratibu wa zoezi la anuani za makazi.

 Zoezi hilo limehudhuria na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya, Katibu wa Chama, Katibu wa Mbunge, Diwani wa kata ya Kakonko, Wakuu wa Taasisi za Serikali na mashirika , Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri, Viongozi wa dini na Wananchi.

Zoezi la uchukuaji wa taarifa kwa kila nyumba litaanza tarehe 21.03.2022 na kuchukua siku 10  ambapo mfumo wa anuani za makazi una manufaa makubwa ikiwemo kuchangia kuimarisha ulinzi na Usalama, Kutengeneza ajira, kuwezesha kufanyika biashara Mtandaoni, kuwezesha mipango na tafiti kufanyika kwa tija na kurahisisha utoaji na upelekeaji wa huduma kwa Wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa