• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA KAKONKO ATOA WITO KWA MAHAKAMA KUTOA ELIMU YA SHERIA KWA WANANCHI.

Imetumwa: February 3rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Evance Mallasa ametoa wito kwa mahakama ya Wilaya ya Kakonko kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya taratibu za kuzingatia na kufuata ili waweze kutatua migogoro yao ya mashauri ya ndoa, talaka, ardhi, mirathi na kutambua taratibu za dhamana.

Amesema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya Sheria yaliyofanyika katika majengo mapya ya Mahakama ya Wilaya ya Kakonko eneo la Kanyamfisi Februari 01, 2023.

 Wakati akitoa salamu ameitaka idara ya Mahakama kuendelea kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya taratibu za kufuata wanapotaka kufika Mahakamani kwani kuna baadhi ya Wananchi wanahofia kufika mahakamani kupata haki zao kwa kuhofia tu kwamba wanaweza kufika wakageuziwa kibao na kuwekwa ndani.

Ameendelea kusema kuwa mahakama inayo wajibu wa kuendelea kuwaelimisha wananchi kwa vipindi mbalimbali kupitia vyombo ya habari  na mitandao ya kijamii kwani  wananchi watakapokuwa na Elimu ya kutosha watakuwa na uelewa kuwa mahakamani ni sehemu ya amani na inayosaidia wananchi.

Aidha ameitaka mahakama kupunguza muda wa kusikiliza kesi ambazo ziko mahakamani bali wajikite katika kutafuta namna ya kusikiliza kesi hizo na kuokoa muda wa kuzisikiliza ili kuendelea kufanya majukumu mengine ya kimaendeleo.

Vilevile ameitaka idara ya Mahakama kuepuka na kujihusisha na vitendo vya rushwa na amewataka Mahakimu pamoja na Watendaji wote kwenye muhimili wa Mahakama kuzingatia misingi ya maadili ya kazi ili waweze kutenda haki kwa Wananchi.

Kwa upande mwingine amevielekeza vyombo vya Usalama na taasisi zingine kama TRA, TAKUKURU, Polisi na Uhamiaji kuendelea kutenda haki kwa Wananchi na kuzuia wale  wanaotumia nafasi kuzulumu haki za wanyonge na kuwapatia haki wale wenye nguvu za kifedha, lakini pia wasiruhusu wale wasio na mamlaka kukosa haki zao na kuwapatia wale wenye mamlaka. kwa kuzingatia hayo watakuwa wanatenda haki kwa wananchi , hivyo Wananchi watakuwa na uelewa mzuri kwa kuwa wanatenda haki.

Naye Hakimu mfawidhi Wilaya ya Kakonko Mhe.Ambilike Kyamba ameeleza katika maadhimisho ya mwaka huu 2023 ya wiki ya Sheria Mahakama kwa kushirkiana na Takukuru, Jeshi la polisi, Uhamiaji na Ustawi wa jamii wamefanikiwa kutoa Elimu ya Sheria kupitia mada mbalimbali katika Shule ya Sekondari Kanyonza, Donnybrook, Kakonko Sekondari, Kakonko wasichana, Muhange Sekondari na Kabare senta. Aidha Mahakama imefanikiwa kutoa Elimu kwa wajumbe wa baraza la kata la Kasanda na Kanyonza, hivyo Wananchi wengi wameelimishwa kuhusu mambo muhimu ya kisheria.

Pia Mahakama imeshiriki katika vipindi ya Radio kwizera kutoa Elimu na kuwasaidia Wananchi kuendelea kufaidika na Elimu ya Sheria.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu kwani ni wajibu wa mahakama na wadau.”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa