• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

RPC KIGOMA AWASISITIZA VIONGOZI KAKONKO KUSHIRIKIANA KUHAKIKISHA UHALIFU UNAONDOKA NA WAUMINI KUFUATA TARATIBU ZA SERIKALI.

Imetumwa: April 3rd, 2024

Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma, Filemon Makungu amewataka Viongozi kushirikiana na jeshi la polisi ili kuhakikisha uhalifu unaondoka huku akiwasisitiza viongozi wa dini kuwaambia waumini wao kufuata sheria na taratibu za Serikali pamoja na kuzingatia Imani zao.

Kamanda Makungu ameyasema hayo alipofanya kikao na kukutana na Viongozi mbalimbali akiwemo Kaimu Katibu Tawala, Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Viongozi wa wa Jeshi la Polisi ngazi ya Wilaya na Vituo, Jeshi la akiba, Watendaji wa Kata na Vijiji, Wenyeviti wa Vijiji na kamati ya maridhiano ambayo imehusisha Viongozi mbalimbali wa madhehebu ya kikiristo pamoja na waislamu.

Akizungumza katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Jumanne Aprili 02, 2024 Kamanda Makungu ameeleza kuwa kwa mujibu wa sheria namba 07 ya Serikali za Mitaa na vifungu vyake, Viongozi wanapaswa kuhakikisha usalama upo kwa Wananchi pamoja na mali zao.

Hata hivyo amesisitiza kuwa Wananchi wanapaswa kufuata sheria na maelekezo ya Serikali na endapo wanajitokeza watu wakorofi, vikao vifanyike ili kuwajadili na kuwachukulia hatua za kisheria.

“Ninyi wote ni watekelezaji na wasimamizi wa sheria huko hakikisheni wananchi wanatii katiba na sheria ya nchi”, ameeleza kamanda Makungu.

Aidha Kamanda Makungu ameeleza kuhusu suala la wahamiaji haramu hususani katika Mkoa wa Kigoma ambao unapakana na nchi jirani ya Congo, Rwanda na Burundi kuwa wahamiaji wanatakiwa kuingia Tanzania kwa kufuata taratibu za nchi.

Kamanda makungu ameeleza kuwa raia yeyote wa Burundi au nchi nyingine anayekuja Tanzania anatakiwa awe na kibali maalum kutoka kwao. Na akifika Tanzania mfano anakuja kutafuta kibarua cha kulima au kufanya kazi akifika kwa Mwananchi au mwenyeji wake anatakiwa kupelekwa Mwenyekiti wa Kijiji au kitongoji ili kukaguliwa iwapo ana vibali.

Baada ya hapo anatakiwa apelekwe kwa Afisa Uhamiaji ili kupewa utaratibu wa kukaa naye kisheria na siku anataka kuondoka anatakiwa apelekwe kwa Mwenyekiti wa Kijiji au kitongoji kuona iwapo ana madai au amefuata taratibu zote.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma ameeleza viongozi wamepewa maeneo ya utawala kuyaongoza na kuhakikisha usalama wa watu na mali zao ili anashangazwa anapofika sehemu na kuwauliza viongozi kuhusu taarifa za wahamiaji haramu na wao kusema hawajui hivyo kuhoji nani aulizwe sasa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko, Ndaki Stephano Mhuli amemshukuru Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kigoma kwa kufanya ziara Wilayani Kakonko na kueleza kuwa wapokea maelekezo na watafanyia kazi kwa mujibu wa sheria na maelekezo ya Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa