Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Walimu wawezeshaji wa mradi wa IPOSA Integrated Programme for out of School Adolescents (Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana) kutoka Shule ya Msingi Maendeleo, kasanda, Gwarama, na Kasuga wameshiriki Mafunzo ya siku mbili Januari 05-06, 2023 yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.
Dr.Sempeho Siafu Mratibu wa Mradi wa IPOSA kitaifa amesema lengo la mradi huu ni kuwafikia vijana ambao wako nje ya mfumo wa Elimu rasmi na wale waliokata tamaa ili waweze kuwajengea uwezo kupitia stadi mbali mbali za Maisha na ujasiliamali kama ufundi selemala, ushonaji wa nguo ,utengenezaji wa sabuni na ufundi ujenzi ili waweze kujikomboa kiuchumi.
Kwa upande wake mwezeshaji wa Mafunzo Bi. Mugabe Mtani kutoka Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima amesema wawezeshaji wa mradi huo wanatakiwa kuongeza kasi ya kusajili Wanafunzi katika mradi wa IPOSA na kuwajengea uwezo pia kufanya uhamasishaji katika ngazi ya Jamii kupitia viongozi wa Serikali kama Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji, Waheshimiwa Madiwani, na Watendaji wa Kata na Vijiji ili kuhamasisha vijana na wananchi juu ya umuhimu wa mradi wa IPOSA.
Ameendelea kusema wawezeshaji wa mradi huu washirikiane wao kwa wao pia washilikishe Vyuo vya Ufundi (SIDO/VETA), Taasisi zisizo za Kiserikali, Mashirika ya Kitaifa, Taasisi za Kibenki na Mashirika ambayo yapo katika maeneo yao ili waweze kupata michango ambayo itawasaidia katika kuendesha shughuli mbali mbali za mradi wa IPOSA. Hivyo amewasisitiza kutengeneza bidhaa bora ambazo zitapata na soko na kuchangia uchumi wao kuongezeka na uchumi wa Halmashuri husika.
Aidha Fred Juma kutoka OR- TAMISEMI amesema amefarijika kwa namna Mafunzo yanavyoendeshwa hivyo anatarajia kuona mabadiliko chanya katika Shule ambazo zinaendesha Mradi wa IPOSA.
Naye Tumaini Hassan kutoka Wizara ya Elimu OR-TAMISEMI amesema baada ya mafunzo hayo kutolewa Walimu Wawezeshaji wa vituo husika wahakikishe wanatoa Mafunzo ya ujuzi wa Stadi mbali mbali za Maisha kwa vijana ambao wako nje ya mfumo wa Elimu rasmi ili waweze kujikomboa kiuchumi. Aidha amelishukuru Shirika la UNICEF kwa kufadhili mradi huo.
Mradi wa IPOSA umefadhiliwa na Shirika la UNICEF kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI. Vituo vinavyoshiriki Mafunzo ni pamoja na Shule ya msingi IPOSA Maendeleo, Gwarama, Kasanda na Kasuga.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa