• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

SERA YA AFYA MOJA YALENGA KUUNGANISHA TIMU ZA MAAFA KATIKA KUKABILIANA NA MAAFA.

Imetumwa: April 19th, 2024

Kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha nchini Tanzania na kushika kasi mwezi Januari 2024, madhara yamekuwa yakijitokeza kwa Wananchi ikiwemo nyumba kubomoka, mazao kuharibika, maeneo ya biashara kuathirikia na baadhi ya watu kupata majeraha na vifo hivyo kuleta maafa kwa jamii.

Serikali ya Tanzania imeandaa mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa maafa (2022-2027) ikidhamiria kulinda maisha ya watu na mali zao kutokana na maafa.

Akitoa dibaji katika mkakati wa Taifa wa usimamizi wa maafa (2022-2027) Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano waTanzania ameeleza kuwa Mkakati huu umeandaliwa kwa kuelewa kwamba mafanikio ya mipango yote ya maendeleo yanahitaji kulindwa dhidi ya madhara ya matukio ya maafa.

Hivyo Mkakati umeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025, Mpango Elekezi wa muda Mrefu 2011/12-2025/26), Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano na sera, mikakati na mipango mbalimbali ya kisekta. Aidha, mkakati unawiana na mifumo ya kikanda na kimataifa inyohusu usimamizi wa maafa kama vile mkakati wa Sendai wa kupunguza hatari za Maafa 2015-2030, Malengo ya Maendeleo Endelevu, Mkataba wa Afrika wa kupunguza hatari za Maafa.

Kwa mujibu wa mkakati wa Taifa wa usimamizi wa maafa (2022-2027) maafa maana yake ni madhara yanayotokana na janga ambayo yanahusisha uharibifu wa mfumo wa kawaida katika jamii, kusababisha vifo, majeruhi, madhara ya kisaikolojia, upotevu au uharibifu wa mali, mifumo mbalimbali ya kiteknolojia na huduma za kiuchumi na kijamii au mazingira kwa kiwango chochote ambapo jamii iliyoathirika haiwezi kukabili kwa kutumia rasilimali zake bila msaada kutoka nje ya jamii hiyo.

Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Shirika la Chakula duniani (FAO) wameandaa na kutoa mafunzo Mkoani Kigoma kwa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza na Wilaya ya Kakonko kwa Timu ya maafa ya Wataalam ili kueleza dhana ya Afya moja na kuwajengea uwezo.

Mafunzo hayo yamefanyika Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma kuanzia Aprili 16, 2024 hadi Aprili 19, 2024 ikihusisha Wataalam kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Waratibu wa maafa, Wataalam wa mifugo, Wataalam wa Mazingira, Wataalam wa maabara, Mratibu wa ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa ya mlipuko (eIDSR FP), Watalam wa misitu na Maafisa mawasiliano.

Afya moja maana yake ni dhana inayotumika kuweka ushirikiano baina ya sekta zinazohusika na afya ya binadamu, wanyama na mazingira, ili kuimarisha uratibu na usimamizi katika utendaji na kupanga mikakati ya pamoja inayolenga kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na mlipuko ya magonjwa na visumbufu vya mimea na mazao ikiwemo madhara ya majanga yanayovuka mipaka na yanayoweza kusambaa kwa muda mfupi, usugu wa madawa, usalama wa chakula na lishe na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na mmoja wa waratibu wa programu ya Afya moja Bi.Valentina Sanga wakati akitoa mafunzo hayo kwa washiriki ameeleza kuwa katika ngazi ya mkoa na Wilaya kumekuwa na majanga yanayojitokeza ambapo wataalam wamekuwa wakiyakabili majanga hayo kisekta hivyo dhana ya Afya moja inalenga kuunganisha nguvu ili majanga yanapojitokeza timu ya maafa ifanye kazi kwa pamoja hivyo kuunganisha utaalam, kuokoa muda na rasilimali fedha na kuweza kuifikia jamii kwa wakati na kupata mrejesho.

Mkoa wa Kigoma umekuwa ukiingiliana na nchi jirani za Kongo, Rwanda na Burundi hivyo kuwa katika hatari ya kupata magonjwa ya kuambukiza kutokana na binadamu, wanyama na mimea.

Kwa mujibu wa ripoti ya Afya moja Tanzania kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Overview of one health platform in Tanzania), 60% ya magonjwa duniani yanatokana na wanyama. Aidha katika miongo mitatu imebainika kuwa 75% ya magonjwa ya binadamu yametokana na wanyama.

Wataalam walioshiriki kufundisha mada mbalimbali ni pamoja na Profesa Sharadhuli Kimera, Dr.Abubakar Shabani Hoza, Bi.Valentina Sanga, Justine Assenga, George Mrema, Salum Nyanga na Samwel Mngumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa