• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

Wanafunzi wenye mahitaji maalum wang'ara kwenye mashindano

Imetumwa: July 5th, 2022

Kuna usemi usemao ‘disability is not inability’ kwa tafsiri isiyo rasmi ina maana kuwa na ulemavu siyo kukosa uwezo wa kutenda jambo. Zipo sababu mbalimbali zinazosababisha ulemavu chache kati ya hizo ni  ajali, magonjwa, na kurithi  vinasamba. Katika halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kuna jumla ya shule za msingi 59. Kati ya shule hizo 44 ni shule zenye Watoto wenye mahitaji maalum wenye viwango vidogo vya ulemavu ambapo shule zinazotengeneza ujumuishi ni 39 na zenye vitengo ni 5.

 Kwa sasa jumla ya Watoto waliosajiliwa na kupata ruzuku ya chakula kila mwezi ni Watoto 293 kwa wilaya nzima. Hii ni hatua kubwa iliyofikiwa katika kipindi cha miaka 7 kulingana na hali ilivyokuwa tete siku zilizokwisha.

Kihistoria Kitengo cha Elimu  maalum kakonko kilianza mwaka 2016 kikiwa na wanafunzi 8 ambapo wavulana walikuwa 6 na wasichana 8 wote wakiwa na ulemavu wa akili wakifundishwa na waalimu 2.

Mwaka 2017 idadi ya wanafunzi iliongezeka na kufikia wanafunzi 11, wavulana 9 na wasichana 2. Kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa uliokuwepo  katika shule ya msingi Kakonko uongozi wa elimu Kakonko uliomba vyumba 2 vya madarasa na ofisi moja kutoka Kanisa la Katoliki Kakonko ili kuweza kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Mwaka 2018 wanafunzi 8 walisajiliwa hivyo kuleta jumla ya wanafunzi 19. Wanafunzi walikuwa wanafundishwa lakini hawakuwa na fungu la chakula kutoka Serikali kuu. Halmashauri ililazimika kutumia mapato ya ndani kuwapatia chakula Watoto hao. Hatimaye mwezi  Julai, 2018 Kitengo cha Watoto wenye mahitaji maalum kilianza kupata huduma ya chakula cha asubuhi na mchana kwa ruzuku kutoka Serikali kuu.

Mwaka 2020 Halmashauri iliongeza vyumba 3 vya madarasa hivyo kupelekea Wanafunzi waliokuwa wakisoma katika majengo ya shule yanayomilikiwa na Kanisa katoliki  kuhamia shule ya msingi Kakonko hivyo shule ikawa na kitengo na kuwa shule yenye elimu jumuishi. Hadi sasa kitengo kina wanafunzi 43 wenye ulemavu tofauti tofauti ikiwemo Watoto wasiioona, walemavu wa miguu, macho Pamoja na Ngozi.

Rekodi iliyowekwa na Watoto wenye ulemavu kwenye michezo ni ya kupongezwa na haijafikiwa hata na Watoto wasio na ulemavu kwani 2021 katika mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa Watoto wenye ulemavu walipata vikombe viwili vya mshindi wa kwanza kwa riadha maalum na mpira wa goli. Aidha Katika timu ya mkoa iliyohusisha wanafunzi sita kutoka shule ya msingi Kakonko walipata medali 11 za dhahabu. Pia michuano ya ‘Special Olyimpics’ yaliyofanyika Mwanza mwaka 2021 shule ya msingi Kakonko ilitoa mshiriki mmoja ambaye alijinyakulia medali 2 za dhahabu na 1 ya shaba.

Mafanikio haya yametokana na ushirikiano wa Wataalam na Wazazi ambapo kwa kiasi kikubwa kazi iliyofanyika ni kubadili mtizamo wa Wazazi wenye ulemavu ili kukubali changamoto wanazopitia Watoto wao wenye ulemavu hatimaye kuwatoa na kuwapa fursa ya kupata elimu. Ni kweli bado ipo kazi ya kufanya lakini kupitia jitihada za Serikali kwa kipindi cha miaka 7 tangu kitengo kianzishwe mafanikio chanya yamejitokeza katika shule ya msingi Kakonko na shule nyingine kufikia kuwa na shule 44 zinazojumuisha Watoto wenye mahitaji maalum.  Ni wakati sasa jamii iwape nafasi Watoto  wenye mahitaji maalum hususani kwenye taaluma na michezo ili kuibua vipaji na Wataalam ambao watakuwa ni tunu ya Taifa kwa siku zijazo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa