• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI KIGOMA WAHIMIZWA KUPIMA AFYA ZAO NA KUTUMIA DAWA ZA ARV.

Imetumwa: December 2nd, 2022


Mkuu wa Mkoa Kigoma Mhe.Thobias Andengenye amewasisitiza Wananchi Mkoani Kigoma kujitokeza kupima Afya zao mara kwa mara, na wanapogundua wana maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wasisite kufika vituo vya afya ili waanze dawa za kufubaza (ARV).

Amesema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yaliyoadhimishwa Kimkoa Wilayani Kakonko katika uwanja wa Mwenge mwishoni mwa wiki siku ya alhamisi tarehe 01 Desemba 2022.

Katika hotuba yake amewasisitiza Wananchi kujiepusha na zinaa zinazochangia maambukizi makubwa ya Virusi vya UKIMWI (VVU) na kuwahimiza wale watakaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU wasisite kuwashawishi na wenza wao ili wakapime na kutambua hali ya afya zao.

“Ndugu zangu wanaume tuache tabia ya kupima kwa kutumia hadhi ya wake zetu waliopima, kwanza tujenge ustaarabu wa kuambatana na wake zetu kwenda kliniki wanapokuwa wajawazito, Kwa hiyo tupime tujue afya zetu kwa sababu kama tukianza kutumia hizi dawa ni vigumu kujua kama tuna changamoto yoyote ya maambukizi ya VVU”. alisema Andengeye.

Aidha  Dr. Jesca Lebba, Mganga Mkuu wa Mkoa alitoa takwimu ya hali ya maambukizi ya VVU kwa Mkoa wa Kigoma kuanzia Januari hadi Oktoba 2022 kuwa yamepungua kwa  asilimia 2.9 kutoka asilimia  3.4 hivyo jumla ya Wananchi waliogundulika kuwa na  maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ni [G1] elfu tatu mia nne na moja (3,401), kati ya Wananchi  laki moja sabini na tatu mia saba kumi na tisa (173,719) waliopima.

 Dr. Jesca aliendelea kusema kuwa katika Mkoa wa Kigoma kuna vituo 83 vya kutolea huduma ya virusi vya UKIMWI na vituo hivyo vyote vinafanya kazi. Aidha Mkoa una mpango wa kuongeza vituo vingine vya kutolea huduma. Hivyo wananchi waendelee kujitokeza kupima Virusi vya UKIMWI.

Japhet Jerome Mkazi wa Kakonko aliwashauri wanaume wasiogope kwa kuona aibu kwenda kituo cha afya na wenza wao kupima maana wanapojitambua kuwa wana maambukizi ya VVU watajipanga namna ya kuishi.

 








Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa