• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WAHIMIZWA KUWA NA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

Imetumwa: April 15th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Kakonko kanali Evance Mesha Mallasa  amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Gwanumpu wilaya ya Kakonko kwa lengo la kusuluhisha mgogoro wa ardhi kati ya muwekezaji na Wananchi wa kata ya Gwanumpu.

Mgogoro huu wa ardhi umeibuka baada ya Uongozi wa Kijiji cha Bukirilo kumpatia mwekezaji ekari 50 kwa ajili ya kuanzisha mradi wa ufugaji wa kisasa, ambapo hapo awali Serikali ya Kijiji ilitenga eneo hilo kwa ajili ya wafugaji.

Akieleza chanzo cha mgogoro huo Diwani wa Kata ya Gwanumpu Mhe. Toyi Butono alieleza kuwa chanzo cha mgogoro huo ni baada ya Wakulima kukuta mashamba yao yamewekewa bikoni na muwekezaji, hivyo wananchi kuhoji hatima ya maeneo yao ya kilimo.

Mhe. Toyi aliendelea kusema kuwa  tangu awali eneo hilo lilikwisha tengwa kwa ajili ya wafugaji na si wakulima, bali kuna shida kubwa ya wananchi wa  Kata ya Gwanumpu kukodisha mashamba kwa raia kutoka nchi jirani ya Burundi kuendesha shughuli za kilimo na ufugaji hali inayopelekea kuibuka kwa migogoro ya ardhi.

Aidha, Mhe. Toyi aliwasisitiza  Wananchi wa Kata ya Gwanumpu kuwa Wazalendo kwa  Nchi yao kwa kuacha kukodisha mashamba kwa raia kutoka Burundi pamoja na kuacha kuingiza mifugo Nchini Tanzania kutoka Burundi kwa kuzingatia hayo hakutakuwa na changamoto ya migogoro baina ya wakulima na wafugaji.

Akihutubia katika Mkutano wa hadhara uliofanyika mwishoni mwa wiki Aprili 14, 2023, katika kijiji cha Bukirilo kilichopo katika Kata ya Gwanumpu Wilayani Kakonko, Kanali Mallasa alieleza kuwa “Hatutamani tuwe jamii ya wana Kakonko ambao tunafuga nyasi, nyasi hizi tumekaa nazo miaka mingi, tunataka haya maeneo yabadilike yawe sehemu za uwekezaji, sehemu ya kukuza uchumi wetu, Sehemu ambayo hata mdogo wetu ambae hajafanikiwa kwenda shule anajifunza kutoka kwa wenzake wanafanya kitu gani, sehemu ambayo watu wengine  wanapata ajira, ndiyo hasa  msingi ambao Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan alituambia tuhakikishe  maeneo  yetu yanakuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi.’’

Aidha Kanali Mallasa alisisitiza Wananchi  kuendelea kutumia maeneo waliyotengewa na uongozi wa kijiji kwa matumizi ya kilimo na ufugaji  bila kuingiliana ili kuepuka migogoro.

Vilevile alisisitiza Uongozi wa Vijiji kuhakikisha unatenga maeneo ya uwekezaji, kwani serikali imekwisha tenga fedha mahususi kwa ajili ya shughuli za uwekezaji wa kilimo.

“Pochi la mama lipo wazi na fedha kwa sasa zipo na zinatawanywa kila Wilaya, sasa kwa sisi wana Kakonko hatuwezi kujitenga ni lazima tuwe na maeneo ya uwekezaji ili Serikali iweze kuleta  fedha hizo kwa ajili ya uwekezaji wenye manufaa,’’ aliongeza Kanali Mallasa.

Aidha alieleza kuwa serikali kupitia Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Inaendesha programu maalumu ijulikanayo kama “Build Better Tommorow” (BBT) ambapo programu hii imelenga kuwainua vijana kiuchumi ambao wanategemea shughuli za kilimo, programu hii imeanzishwa kwa kuzingatia  asilimia kubwa ya wananchi  nchini wanategemea shughuli za kilimo, ukilinganisha na asilimia ndogo ya  wafanyakazi. hivyo amewaasa vijana kuchangamkia fursa hii adhimu ili kutuma maombi ya kujiunga na programu ya BBT, ambapo vijana watakaochaguliwa watapewa mafunzo kuhusu kilimo bora  kwa muda wa miezi mitatu, baada ya mafunzo hayo watarejea katika maeneo yao na kupatiwa ardhi kiasi cha ekari 10 kwa kila kijana na serikali itawapatia  hati miliki za maeneo hayo pamoja na kugharimia shughuli zote za uendeshaji wa kilimo.

 Kwa upande Mwingine Kanali Mallasa alitoa rai kwa Wananchi kuwa makini na baadhi ya wanasiasa wanaowahamasisha kushiriki vitendo vya uvunjifu wa Amani ikiwemo kushiriki maandamano bila kufuata sheria, kwani viongozi hao wa kisiasa wanawapotosha wananchi kuwa aridhi yao imeporwa na kupewa muwekezaji.  ‘’Hivi sasa tunaelekea kipindi cha uchaguzi Wananchi msitumike vibaya na wanasiasa,mkirubuniwa kuwa aridhi yenu imeporwa na uongozi wa kijiji na kupewa muwekezaji, niwaombe wananchi wote ambao maeneo yenu  yamechukuliwa na akapewa muwekezaji, orodhesheni majina yenu na ukubwa wa maeneo yenu kupitia kwa Mtendaji wa Kata, yanifikie ofisini, nitatenga  siku maalum kufika eneo husika na nitahakikisha kila mmoja anapata haki yake” alisema Kanali Mallasa.

 Baadhi ya viongozi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Afisa ardhi, Kamati ya Ulinzi na usalama na wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa