• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WILAYA YA KAKONKO WATAKIWA KUACHA VITENDO VYA UKATAJI NA UCHOMAJI WA MITI.

Imetumwa: November 25th, 2022


Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa amewasisitiza Wananchi wa Wilaya ya Kakonko kuepuka vitendo vya ukataji wa miti ovyo bila kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali ikiwemo uchomaji wa misitu kwa ajili ya shughuli za mbao na uchomaji wa Mkaa.

Amesema hayo wakati akizindua zoezi la upandaji wa miti katika eneo la Stendi ya Mabasi ya kisasa Kakonko Mjini leo Ijumaa tarehe 25/11/2022 na kutoa wito kwa viongozi wote kupanda miti katika maeneo yao. aliongeza kuwa Taasisi za Serikali, Binafsi, Taasisi za dini, Shule zote na Hospitali wapande miti katika maeneo yao na maeneo mengine yanayofaa kupandwa miti.

“Nataka nitumie fursa hii kutoa wito kwa Mwananchi wote wa Wilaya ya Kakonko kuanzia katika familia kila mmoja wetu ajitahidi kupanda miti katika eneo lake kwa ajili ya kuvuna mbao kuepuka janga la umasikini na kujipatia kipato,” alisema Mallasa.

Aidha ameeleza kuwa Wataalam wa TFS wameleta Mbegu nzuri zinazotumia muda mfupi kustawi takriban miaka 7. Hivyo Mwananchi yeyote ambae atabainika akifanya vitendo vya biashara ya miche badala ya kupanda katika eneo lake hatua za kisheria zitachukuliwa.

Aliongeza kuwa Wananchi wote ambao miti imepandwa katika maeneo yao ya barabara wanapaswa waitunze na kuihudumia kwa kuzungushia uzio ili miti hiyo isiharibiwe na wanyama.

Aidha Mkuu wa Wilaya alitoa rai kwa Wananchi wa Wilaya ya Kakonko kuepuka kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka kwenye vyanzo vya maji ili kuepuka kukosa mvua kwa muda mrefu pamoja na hewa safi.

Kwa upande wake Kaimu Mhifadhi Wakala wa huduma za Misitu Wilaya ya Kakonko (TFS) Paschal Amosi Misita alieleza kuwa katika Wilaya ya Kakonko Mjini imepandwa Miti 522, lakini kwa Mwaka 2022/2023 wamepanga kupanda Miche ya Miti laki mbili (200,000).

Aliendelea kusema Miche hiyo ya Miti itagawiwa kwa Wananchi wote bure ili wakapande katika maeneo yao. Aidha alisisitiza wananchi watakaochukua miche ya Miti watafuatiliwa kuona kama wametekeleza agizo la Serikali la kupanda Miti kwani kumekuwa na tabia ya baadhi ya Wananchi kuchukua miti pasipo kupanda.

Farida Ismail, Mwananchi wa kata ya Kakonko ameeleza kuwa zoezi la upandaji miti amelipokea vizuri na ameahidi kuendelea kuwahamasisha Wananchi kupanda Miti na kuitunza. Uwepo wa miti unachangia upatikanaji wa Mvua na hali ya hewa nzuri. Hivyo anaishukuru ofisi ya Mkuu wa Wilaya na TFS kwa kuendesha zoezi la upandaji miti.

Issa Laurent, Mwananchi wa Kijiji cha Mbizi ameeleza anaushukuru Uongozi wa Wilaya kwa kuendelea kuhamasisha Wananchi kupanda miti katika maeneo yao. Kwa upande wake ameeleza kuwa amehamasika na zoezi hilo na kuahidi kwenda Hifadhi ya TFS kuchukua Miche ya Miti na kwenda kupanda.  Kwani miti hiyo italeta manufaa kwa ajili ya kizazi cha baadae.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa