• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WAHIMIZWA KUSIMAMIA ZOEZI LA UPATIKANAJI WA CHAKULA SHULENI.

Imetumwa: February 3rd, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Mhe.Fideli Ndelego amehimiza Watendaji wa Kata na vijiji, Maafisa Elimu Kata pamoja na Walimu Wakuu wa Shule kwa kushirikiana na kamati za wazazi Shuleni wahakikishe  Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari wanapata chakula Shuleni.

Amesema hayo katika kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika mwanzoni mwa mwezi Februari tarehe 02, 2023, katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Baraza la Madiwani liliwashirikisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya, Kaimu katibu Tawala Wilaya ya kakonko, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Waheshimiwa Madiwani, Viongozi wa vyama vya Siasa, Wakuu wa Divisheni na Vitengo, Watendaji wa kata, Viongozi wa Dini pamoja na Wananchi.

“Wananchi wa Wilaya ya Kakanko wanatakiwa kuwa na utaratibu wakuwapatia Watoto chakula Shuleni na kuwapeleka Shuleni bila kusukumwa, hatutakuwa tayari kuona Mzazi anamkataza mtoto wake kupata chakula Shuleni” 

Ameendelea kusema lengo la kuwepo kwa Baraza la Madiwani ni kuendeleza usitawi na maendeleo ya Wananchi wa Kakonko. Hivyo Madiwani wanaahidi kushirikiana, kushikamana na Wananchi ili kuleta mabadiliko na maendeleo chanya katika Wilaya ya Kakonko. Aidha baraza la Madiwani limewataka Wazazi wote ambao bado hawajawapeleka Watoto Shule kuhakikisha wanawapeleka pia viongozi waendele kuhamasiha jamii juu ya umuhimu wa Elimu kwa  kuwapatia Watoto haki yao ya msingi ya Elimu.

Kwa upande wake Kanali Evance Mallasa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ameeleza kila Shule inatakiwa kutoa huduma ya chakula kwa wanafunzi angalau mlo mmoja kwa siku, hivyo Wazazi/Walezi wanao wajibu wa kuchangia chakula Shuleni ili Watoto wapate huduma ya chakula. Amesisitiza kila Shule iwe na shamba darasa kwa ajili ya kulima mazao ya Chakula na kila mwanafunzi apande angalau mti mmoja wa matunda ili Watoto wawe na afya bora.

Alihitimisha kwa kusema jamii bado ina mwamko duni juu ya umuhimu wa Elimu kwani mpaka sasa katika zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza Wilaya ya Kakonko bado haijafikisha asilimia 100%. Hivyo Watendaji wa kata na vijiji, Maafisa Elimu Kata pamoja na Walimu wakuu wa Shule wahakikishe Watoto wote ambao wamefikia umri wa kuanza Shule waandikishwe.

 “Sisi Viongozi tumepata fursa yakuweza kuelewa umuhimu wa Elimu tutumie nafasi hii kuweza kuwaelimisha na wenzetu”

Naye Afidhi Ramadhani Mtendaji wa Kata ya Katanga amesema kuwa kutokana na wazazi kutokuwa na uelewa juu ya umuhimu wa Elimu ndiyo sababu ya kutowapeleka Watoto wao Shule na badala yake kuwapeleka kwenda kufanya kazi za ndani, hivyo kama viongozi wanaowajibu wakuendelea kutoa Elimu kwa wazazi/walezi kwani wengi wao wamekuwa na dhana kwamba wengi waliosoma bado hawaja ajiliwa kupitia dhana hiyo wataendelea kuwa na nguvu kazi isiyokuwa na Elimu

Mkazi wa Wilaya ya Kakonko Naftali Kilaha amesema  Wazazi wengi wamekuwa na dhana kwamba hawana uwezo wa kuwapeleka Watoto wao Shule na badala yake kuwashauri kufanya vibaya katika Masomo yao na kuwapeleka mjini kufanya kazi za ndani pia kuwashauri Watoto wa kike kwenda kuolewa jambo ambalo linasababisha matatizo kwa wazazi na jamii kwa ujumla.

Naye Afisa uchunguzi TAKUKURU Ndugu Nelson Kailembo Wilaya ya Kakonko ametumia fursa ya Mkutano wa Baraza la Madiwani kutambulisha Programu ya “TAKUKURU Rafiki” kuwa ni program iliyoanzishwa na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kwa lengo kuongeza ushiriki wa kila mwananchi na wadau katika kuzuia rushwa katika utoaji wa huduma kwa jamii na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa