• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI WAHIMIZWA KUZINGATIA MAFUNZO.

Imetumwa: December 15th, 2022

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Michael Faraay amewahimiza Watumishi Wapya kuzingatia na kuyaishi yale ambayo watajifunza pia kuwa na mpango kazi utakao wasaidia kuendeleza majukumu yao pale watakapo kuwa katika vituo vyao vya kazi.

Alisema hayo mwisho mwa wiki hii wakati akifungua Mafunzo elekezi ya siku mbili Disemba 15 -16, 2022, kwa Watumishi wapya kutoka idara ya Afya, Elimu, na Utawala ambapo mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.

Kwaupande wake Afisa Utumishi Wilfred Ntagaye amesema kuwa lengo kubwa la Mafunzo ni kuwajengea uwezo Watumishi Wapya kufanya kazi katika misingi ya maadili ya utumishi wa umma kwani Mafunzo hayo yatawasaidia Watumishi ambao ndio watoa huduma kwa Wananchi na kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji kazi wao.

Radisilaus Ibrahim Kamanda Mkuu wa Takukuru Wilaya ya Kakonko amewataka Watumishi Wapya kutojihusisha na vitendo vya rushwa kwani lengo la Serikali ni kuja kuwatumikia Wananchi wa Wilaya ya Kakonko na kuhakikisha kila Mwananchi anapata maendeleo kwa haraka kwa kuzingatia Huduma zinazotolewa kwa haki na usawa bila kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Aidha katibu wa Afya Kakonko Gwamaka Edison amewasisitiza Watumishi Wapya kuutumia umoja wao kama chombo cha kuwaunganisha na kushikamana katika matukio ya kikazi na kijamii.

Naye Afisa maliasili Wilaya ya Kakonko Bosco Huruma  amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji kusimamia vyanzo vya maji na kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya utunzaji wa Mazingira kwani wao ndio wenye dhamana ya kusimamia Mazingira kikamilifu hivyo  amewaomba kutunga Sheria ndogo ndogo ili kuthibiti majanga ya moto kwa kuunda Kamati ambazo zitasaidia kutoa Elimu kwa Wananchi juu ya madhara ya uchomaji wa moto.

Kwaupande wake Afidhi Ramadhani Mtendaji wa Kata ya Katanga ambae ni mmoja wa Watumishi Wapya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko amesema kuwa kupitia mafunzo hayo wamejifunza mambo mengi hivyo ufanisi wao wa kazi utaenda kuongezeka katika utendaji kazi, vilevile wameahidi kwenda kufanya kazi ambayo itakuwa na tija kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko na Serikali.

‘’Tutaendelea kuwa wabunifu kwa kutumia Elimu rasimi na isiyo kuwa rasimi kuhakikisha tunafanya kazi kwa makini na kuleta tija katika kazi zetu lengo kubwa ni kuwasaidia Wananchi wa Wilaya ya Kakonko’’ Amesema Afidhi Ramadhani.

Eliwaza Petro Mwalimu wa Sekondari Buyungu ameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kwa kuaandaa mafunzo hayo ambayo yatawajenga katika utendaji kazi kwa kuzingatia misingi ya maadili ya kiutumishi pia amewapongeza wakufunzi kwa kutoa mafunzo hayo kwani hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza na mafunzo yameisha salama.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa