• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WAZAZI WAPEWA SIKU 2 KUWAPELEKEA WATOTO SHULE WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023.

Imetumwa: January 19th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Evance Mallasa Ametoa siku mbili kuanzia tarehe 19-21 Januari, 2023 kwa Wazazi ambao hawajapeleka watoto wao Shuleni kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanapelekwa shuleni.

Amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya umaliziaji wa vyumba vya madarasa Shule ya Sekondari Dr. Mpango na Ikambi mwishoni mwa mwezi Januari, 2023.

Aidha Kanali Mallasa amewataka Watendaji wa Kata kuhakikisha wazazi wanawapeleka watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwani hakuna sababu yakuendelea kukaa na watoto nyumbani hali yakuwa madarasa yapo tayari. Ameendelea kusema kwa mzazi ambae ataendelea kukaidi kumpeleka mtoto wake shuleni hatua za kisheria zichukuliwe ikiwemo kuwafikisha mahakamani.

Mkuu wa Shule ya sekondari Dr.Mpango Boniface Kayombo amesema kuwa upatikanaji wa madarasa hayo yatasaidia kukuza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi kwani kabla ya kupatikana kwa madarasa hayo hali ilikuwa ngumu.

Edga Dennis Abdallah Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Dr.Mpango amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani kwakuwajengea Shule karibu kwani walikuwa wanatembea umbali mrefu ambao ulikuwa unasababisha kutofika shule na badala yake kuishia njiani.

Naye Safina John Mabano Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Dr.Mpango ameishukuru Serikali kwa kujenga shule karibu kwani walikuwa wakikutana na vikwazo vingi hivyo kuahidi kufaulu katika masomo yao. 

Fredrick Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Dr.Mpango amewaomba wazazi kuonyesha ushirikiano wa kuwapeleka watoto shule ili waweze kutimiza ndoto zao kwani wazazi wamekuwa wakiwanyima haki ya kupata elimu.

Wakazi wa Kijiji cha Kazilamihunda iliyopo katika kata ya Kasanda wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea miradi ya maendeleo ikiwemo Shule hivyo wameahidi kuendelea kushirikiana na Walimu pia kuendelea kutoa Elimu kuhakikisha wanapeleka watoto wao shule waweze kupata Elimu itakayo wasaidia baadae, vilevile wamewashauri wazazi wenzao ambao bado hawajapeleka watoto shule na kuacha kuwaficha watoto badala yake kuwatuma kwenda kufanya kazi za ndani.

Hadi sasa wazazi nane (8) Wamefikishwa ofisi ya Kata ya Kasanda kutoa maelezo ya sababu za kushindwa kuwapeleka watoto wao shule kuripoti.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa