Mwenyekiti wa wazee wilaya ya Kakonko ndugu Mbonimpa Gerald Bisama ameiomba jamii kutokuwadai kodi za nyumba wazee ambao wamepanga katika maeneo yao. Akisoma risala kwa niaba ya wazee wa Wilaya ya Kakonko mbele ya mgeni rasmi Col.Hosea Ndagala, mwenyekiti amesisitiza Jamii kuwatunza wazee kwani kwa sasa 46% ya wazee wanawatunza watoto yatima badala ya wao kutunzwa.
Aidha ameiomba Serikali kutoa pensheni ya Jamii kwa wazee ili kutimiza ahadi iliyotolewa na Serikali mwaka 2008 ambapo tayari Serikali ya Zanzibar imeanza kutoa pensheni jamii kwa wazee. Vilevile wazee wameomba wakati mishahara inapopanda na pensheni za wazee zipande. Maadhimisho ya siku ya wazee kiwilaya yamefanyika katika kata ya Kasanda Wilayani Kakonko hivi karibuni na kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Co.Hosea Ndagala mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Christopher Bukombe na wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo waliofadhili siku hiyo ya wazee ambayo ni mashirika yanayohudumia wakimbizi katika kambi ya Mtendeli wakiwemo Help age International na TCRS.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa