• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe |
Kakonko District Council
Kakonko District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Mawasiliano
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Usafishaji Na Mazingira
        • Elimu Msingi
        • Elimu ya Sekondari
        • Afya na Ustawi wa Jamii
        • Maji
        • Maendeleo ya Jamii
        • Utumishi na Utawala
        • Fedha na Biashara
        • Maliasili, Ardhi na Mazingira
        • Kilimo cha Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
        • Ujenzi na Zimamoto
      • Vitengo
        • Ugavi na Manunuzi
        • Tehama na Habari
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ufugaji Nyuki
        • Uchaguzi
        • Sheria
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Livestock
    • Fisheries
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Usimamizi
      • Elimu Afya na Maji
      • Huduma za Kiuchumi Ujenzi na Mazingira
      • Udhibiti wa UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
        • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYANI KAKONKO WATAKIWA KUSIMAMIA VIZURI MATUMIZI BORA YA ARDHI.

Imetumwa: January 13th, 2025

Wenyeviti wa Vijiji  na  Vitongoji  kutoka katika kata 13 zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko wamejengewa uwezo kwa kupata mafunzo yatakayo wasaidia kujua majukumu na mipaka ya nafasi zao katika utekelezaji wa majukumu yao  ya kila siku kwa wananchi wao. Mafunzo hayo yamefanyika  kwa mda wa siku mbili katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Wilayani Kakonko ambapo yametamatika leo Tarehe 13,Januari 2025.

Akifunga Mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa,amewataka wenyeviti hao kusimamia vizuri matumizi bora ya ardhi, ambapo ameeleza kuwa kumekuwepo na changamoto ya migogoro ya ardhi katika maeneo yao kwa hali hii imekuwa ikichangiwa na baadhi ya viongozi wa ngazi za vijiji ambao wamekuwa wakikosa uandilifu katika kutimiza majukumu yao. Hivyo ameendelea kuwasisitiza kwenda kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Aidha Col.Mallasa amewapongeza wenyeviti hao kwa kuchaguliwa kuwa wenyeviti wa mitaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Novemba 27  2024 na kueleza kuwa hana wasiwasi na viongozi hao waliochaguliwa kwani kama wilaya wataendelea kutoa ushirikiano kwa pamoja katika kutekeleza majukumu ili kuijenga Kakonko.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndg Ndaki Stephano Muhuli, ameeleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kwa lengo la kuwakumbusha na kuwaelekeza majukumu mbalimbali ya utendaji wa shughuli za kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia sheria,kanuni na miongozo ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Hata hivyo amewataka kwenda kusimamia fedha za serikali zinazokusanywa katika maeneo yao na kutoa taarifa fedha zinapoingia kwani katika vijiji vyao kuna vyanzo vingi vya ukusanyaji wa mapato. Ameendelea kuwasisitiza kuendelea kutatua kero za wananchi katika maeneo yao hivyo waendelee kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabiri wananchi.

Naye Bi.Sarah Kilagane, Mwezeshaji kutoka Chuo cha serikali za mitaa Hombolo, amezungumzia majukumu ya mwenyekiti wa kijiji ikiwemo kuwa mwenyekiti wa vikao vya kijiji, kuwakilisha wananchi katika kamati ya maendeleo ya kata na kutatua migogoro mbalimbali ya wananchi ambayo haina ulazima wa kufika katika mamlaka au ngazi nyingine.

Baadhi yao wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuahidi kwenda kutekeleza yale yote waliyoelekezwa kwenye mafunzo ikiwa nikuendelea kutatua changamoto za wananchi na kusimamia fedha za serikali pamoja na matumizi bora ya ardhi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - WAKUSANYA MAPATO January 30, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. June 18, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA YA WAOMBAJI NAFASI YA UKUSANYAJI MAPATO WALIOITWA KWENYE USAILI January 23, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA VITENDO - WAOMBAJI KAZI YA DEREVA II November 17, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    April 29, 2025
  • UANZISHWAJI WA MFUMO WA UTHIBITI UBORA WA SHULE WATAJWA KUWA CHACHU KATIKA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA KIUTENDAJI..

    April 17, 2025
  • JIMBO LA BUYUNGU LABADILISHWA JINA NA KUITWA JIMBO LA KAKONKO.

    March 13, 2025
  • MHE.KAMAMBA AWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO NA BIASHARA PAMOJA NA KUJIENDELEZA KIELIMU.

    March 03, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkurugenzi afafanua mikakati ya kuendeleza zao la parachichi ikiwemo kugawa mashamba kwa wananchi.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Watendaji
  • Ukaguzi wa Miradi Kakonko
  • Lori jipya la Halmashauri laongeza kasi ya utekelezaji Miradi ikiwemo mradi wa Ufyatuaji tofali
  • TASAF kuibua ajira Kakonko
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko - FACEBOOK account
  • Habari motomoto za magazeti kila siku
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO- INSTAGRAM ACCOUNT
  • WANAFUNZI WILAYA YA KAKONKO WALIOPANGIWA SHULE KIDATO CHA KWANZA
  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WILAYA YA KAKONKO 2022

Viunganishi linganifu

  • Poralg
  • Public Service Management and Good governance
  • Necta
  • Tanzania portal
  • Kigoma Region Website
  • Tangazo la nafasi za kazi
  • Matokeo kidato cha nne 2018/2019 haya hapa
  • Balozi wa Norway akabidhi vifaa vya mifugo kakonko
  • Bunge la Tanzania
  • kakonko tv
  • Mapinduzi sekta ya elimu Kakonko
  • halmashauri ya wilaya ya kakonko - habari na mawasiliano
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA 2 MWAKA 2022

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 3

    Simu: +255(028) 2988881

    Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881

    Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz

Mawasiliano

   

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma
    • Kanusho

Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa