Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko anapenda kuwaarifu waombaji wa kazi wa nafasi ya Mwandishi Mwendesha Ofisi II na Dereva Daraja la II waliofanya usaili kuanzia tarehe 19/06/2025 hadi tarehe 21/06/2025 kuwa waombaji waliofaulu ni kama walivyoorodheshwa kwenye tangazo hapa chini. Aidha waombaji waliofaulu usaili wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri Mkurugenzi Mtendaji (W) wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ndani ya siku saba kuanzia tarehe ya tangazo hili wakiwa na vyeti halisi vya kidato cha nne/sita na vyeti vya taaluma ili kuendelea na taratibu za ajira. Barua ya kupangiwa vituo vya kazi zitatolewa baada ya kukamilika kwa taratibu za Ajira.
Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi zilizopangwa.
Tangazo la kuitwa kazini 21.6.2025.pdf
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko
Anuani ya Posta: P.O.BOX 3
Simu: +255(028) 2988881
Simu ya Mkononi: +255(028) 2988881
Barua Pepe: ded@kakonkodc.go.tz
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa