Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa amehitimisha bonaza la Michezo mbalimbali Desemba 8, 2022 lililokuwa likifanyika katika shule ya msingi Maendeleo na kuwahimiza Wananchi kushiriki katika michezo ili kuepukana na magonjwa nyemewelezi ikiwa ni moja ya shughuli ya kuadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania bara.
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ameongoza zoezi la usafi na kutembelea wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Muganza siku ya Jumatatu tarehe 05.12.2022 ikiwa ni moja ya shughuli katika wiki ya kuadhimisha Uhuru wa Tanzania siku ya Ijumaa Desemba 09.
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Col.Evance Mallasa amekabidhi Tshs.500,000 siku ya Ijumaa tarehe 02 Desemba, 2022 ofisini kwake kwa wajane 10 wa Wilaya ya Kakonko ikiwa ni ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andegenye aliyepokea fedha hizo kutoka kwa Mdau wa Maendeleo ili kuwapatia wajene waliopo katika makanisa.
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa