Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imeanza kutoa leseni kiditali kwa kutumia mfumo wa Tausi ambapo leo Alhamisi Mei 04, 2023 leseni imetolewa kwa mfanya biashara mmoja aitwaye Raurent Gurand Richard kwa niaba ya wafanyabiashara wengine.
Akiwapongeza divisheni ya biashara na viwanda Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli ameeleza kuwa anawapongeza kwa kazi nzuri ambayo wameifanya ikiwa ni utekelezaji wa matakwa ya Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Dr.Samia Suluhu Hassan kutoa leseni zote kupitia mfumo wa kidigatali wa Tausi.
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ameitaka Halmashauri kuongeza nguvu kuimarisha Hospitali ya Wilaya, kuwa na dira na kusimamia rasilimali watumishi kuheshimiana, kuthaminiana na kuonesha upendo kwa wagonjwa,kufuata taratibu za utoaji wa huduma za afya wakati akifunga huduma za madaktari bingwa kutoka Hospitali ya kanda Chato.
Madaktari bingwa kutoka hospitali ya kanda Chato wamehudumia wagonjwa 315 Wilayani Kakonko katika zoezi la siku 5 kuanzia tarehe 24-28 Aprili, 2023 kutibu magonjwa mbalimbali ya Wanawake, watoto, magonjwa ya ndani na oparesheni 7.
Hatimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Haki zote zimehifadhiwa